SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameyasema hayo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi katika hafla ya uzinduzi wa Mfumo Jumuishi wa Kielektroniki (ISQMT) uliofanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.
Amesema kuzinduliwa kwa mfumo Jumuishi wa Kielektroniki wa Viwango wa ZBS utatanua wigo madhubuti wa kurahisisha mchakato wa kukuza ubora wa bidhaa, kuhakikisha uwazi katika udhibiti na kurahisisha huduma kwa wazalishaji, wafanyabiashara na watumiaji kwa ujumla.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Mfumo wa Viwango wa ZBS utaiwezesha Taasisi hiyo ya Viwango Zanzibar kuwa na uwezo wa kufuatilia bidhaa kwa usahihi, kuharakisha utoaji wa vyeti vya ubora na kuwawezesha wadau wote kupata taarifa kwa njia ya kidijitali jambo litakaloongeza ufanisi katika Sekta ya Viwanda na Biashara.
Aidha, Mhe. Hemed amesema Mfumo wa ISQMT umelenga kuweka Mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na nje kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa zinakuwa na ubora na zinakidhi viwango vya Kitaifa na Kimataifa pamoja na kuondoa usumbufu ulikuwepo kwa muda mrefu hasa katika upatikanaji wa huduma kwa uwazi.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewahimiza watendaji wa ZBS kuhakikisha kuwa Mfumo wa ISQMT unatumika kwa ufanisi mkubwa pamoja na kuwataka wafanyabiashara, Wazalishaji na wadau wote wa Sekta ya Viwango kuutumia kikamilifu mfumo huo kwa lengo la kukuza ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini.
Mhe. Hemed ametoa wito kwa wadau wote wa Sekta ya Biashara na Viwanda kushirikiana na ZBS na Taasisi nyengine za udhibiti wa viwango ili kuhakikisha kuwa bidhaa zote zinakuwa na viwango bora na salama kwa matumizi ambavyo vitaiwezesha Tanzania kuwa Taifa lenye ushindani mkubwa katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Zanzibar (ZBS) Ndugu Yusuph Majid Nassor amesema madhumuni ya Kuazimishwa kwa Mfumo wa Viwango Zanzibar ni kuleta ujumuishaji wa wadau wote wanaofanya kazi na ZBS ili kufanya kazi kwa ufanisi na Tija pamoja na kupunguza changamoto mbali mbali katika utowaji na upatikanaji wa huduma.
Yusuph amesema zaidi ya shilingi za Kitanzania Bilioni 1.2 zimewekezwa katika uandaaji wa Mfumo huo kupitia wafadhili Trade Mark Afrika ambao utarahisisha upatikanaji wa huduma kwa njia ya kidijitali kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kanda Afrika Mashariki na Kati bibi Monica Hangi amesema Taasisi ya Trade Mark Afrika kwa Kushirikiana na Shirika la Viwango Zanzibar (ZBS) wameamua kuanzisha mfumo wa viwango Zanzibar kwa lengo la kuboresha mazingira ya ubora na kuweka ufanisi katika kuboresha na kuweka viwango vinavyokubalika Kitaifa na Kimataifa.
Monica anesema kuzinduliwa kwa mfumo huo Zanzibar itaweza kuunganishwa na masoko ya ndani na nje ya nchi, kufanya kazi kwa uwazi, uhakika na kwa haraka jambo ambalo litachangia kuongezeka kwa mapato ya Serikali.
Monica amefahamisha kuwa mfumo huo utakaokuwa na viwango ambavyo vitawasaidia wadau na wazalishaji wa bidhaa Zanzibar kuweza kutengeneza bidhaa zenye viwango vya kufikia na kukidhi matakwa ya ushindani wa Kibiashara katika Masoko ya Biashara ya ndani na nje ya nchi.
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
31-05-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
31-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
31-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
31-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
31-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
31-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
31-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
31-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
31-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
31-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
31-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
31-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
31-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
31-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
31-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
31-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
31-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
31-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
31-05-2026