Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar Alhaj Dkt.Mohamed Said Dimwa,amewasihi waumini wa dini mbalimbali nchini kufuata falsafa na maoni ya aliyekuwa Rais wa awamu ya pili ya jamhuri ya muungano wa Tanzania pamoja na Rais wa awamu ya tatu ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Marehemu Ali Hassan Mwinyi.
Wito huo ameutoa wakati akizungumza katika hitma ya kumuombea marehemu Mzee Mwinyi iliyofanyika katika msikiti wa Donge Pangamaua Jimbo la Donge,amesema kiongozi huyo enzi za uhai wake amekuwa ni mfano wa kuigwa katika maisha yake ya uongozi na baada ya kustaafu kwa kuishi katika misingi ya maadili,uadilifu na ucha Mungu.
Alhaj Dkt.Dimwa,alisema Mzee Mwinyi atabaki katika kumbukumbu na historia ya kipekee katika kulinda,kutetea na kuendeleza misingi ya uongozi bora wenye kufuata matakwa ya kidemokrasia kwa wananchi na alipinga tabia za ubaguzi wa kidini,kikabila na kisiasa.
“Zawadi kubwa ya kumpatia Mzee wetu huko aliko ni kumuombea dua kwa wingi ili Mwenyezi Mungu amjaalie mema,nasi tuendeleze pale alipotuachia kwa kuhakikisha tunaishi katika misingi ya maadili mema ya ushirikiano,upendo na kudumisha amani na utulivu”, alisema Dkt.Dimwa.
Aliwasihi waumini hao na wananchi kwa ujumla kuwarithisha watoto wao misingi ya maadili mema katika malezi yao ya kila siku ili kupata viongozi bora wa sasa na baadae.
Katika maelezo yake Naibu Katibu Mkuu huyo Dkt.Dimwa,alieleza kuwa kila mwananchi ana jambo la kujifunza juu ya maisha ya Mzee Mwinyi harakati za kiungozi,kidini,kitamaduni na kisiasa.
Kupitia hitma hiyo Dkt.Dimwa,alitoa salamu za Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi kuwa anawashukru wananchi wa Jimbo la Donge na majimbo jirani wanaofanya hitma na dua mbalimbali za kumuombea kiongozi huyo Mzee Ali Mwinyi aliyeongoza Serikali zote mbili ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar kwa ujumla.
Katika hitma hiyo iliyoandaliwa na Jimbo la Donge iliudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mwakilishi wa Jimbo hilo Dkt.Khalid Salum Mohamed,Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Rashid Hadid pamoja na Madiwani na wananchi wa jimbo hilo.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
26-10-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
26-10-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
26-10-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
26-10-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
26-10-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
26-10-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
26-10-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
26-10-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
26-10-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
26-10-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
26-10-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
26-10-2025
TAARIFA KWA UMMA
26-10-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
26-10-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
26-10-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
26-10-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
26-10-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
26-10-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
26-10-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
26-10-2025