Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameutaka uongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT) na wanachama wake kuyatumia vyema mafunzo wanayopatiwa ambayo yatawajengea uwezo wa utekelezaji wa majukumu yao ili kuleta mabadiliko ya kiutendaji katika Chama cha Mapinduzi sambamba na kutatua changamoto za wanachama zinapojitokeza
Ameyasema hayo katika ufunguzi wa Semina ya siku moja ya kuwaongezea ujuzi na maarifa Madiwani, Makatibu wa Wadi na Majimbo pamoja wajumbe wa kamati tendaji iliyofanyika katika ukumbi wa Viwanja vya Maonesho Nyamanzi Zanzibar Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.
Mhe. Hemed ameseama moja ya jukumu la UWT ni kutoa elimu kwa wanachama, kuwahamasisha wanawake katika kugombea nafasi za Uongozi, kuishauri Serikali na kutatua changamoto katika jamii kwa lengo la kuweka mustakbali mwema wa Taifa na chama cha Mapinduzi ili kiendelee kushika Dola awamu kwa awamu.
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Uongozi ni kuonesha njia kwa wanowaongoza ili kufikia malengo yaliyokusudiwa na kusema kuwa kufuata maadili ya Uongozi na Utendaji ni jambo la msingi ambalo litasaidia kunyanyua ari kwa wafuasi wa Chama na kuleta maendeleo kwa Jumuiya.
Aidha Mhe. Hemed ametoa wito kwa Viongozi kuzitumia vyema nafasi zao kwa kufuata misingi ya uongozi kwa wanowaongoza ikiwemo nidhamu, uaminifu, uadilifu, unyenyekevu, kujenga umoja, matumizi mazuri ya lugha, kutatua kero na kuandaa viongozi wapya watakaoweza kushika nafasi mbali mbali katika Jumuia.
Sambamba na hayo, Mhe Hemed amesema anatambua kuwa wapo baadhi ya viongozi na watendaji hawana lugha nzuri kwa wanowaongoza hivyo amewataka kujirekebisha na kuachana na tabia hiyo kwani Chama cha Mapinduzi hakitamvumilia mtu yoyote atakae kwenda kinyume na maadili ya Chama, hivyo amewahamasisha wanawake ndani ya Chama Cha Mapinduzi wenye uwezo wa kuongoza kujiandaa na kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali za Uongozi katika Uchagzi Mkuu wa mwaka 2025.
Kwa upende wake Mwenyekiti wa UWT Taifa Bi. Mary Pius Chatanda amezipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kukamilisha vyema na kwa mafanikio makubwa zoezi la sensa la kidigital ambalo halijawahi kutokea nchini ambalo takwimu zake zitalisaidia Taifa katika kupanga mikakati mbali mbali ya kimaendeleo nchini.
Chatanda amewaagiza viongozi ambao wamepatiwa mafunzo hayo kushuka kwa wananchi kusikiliza kero zao zinazowakabili ili kuweza kufanya maamuzi sahihi katika vikao vya chama na Serikali.
Aidha amewataka viongozi wa UWT kuendelea kufanya zoezi la usajili wa wanachama wapya kwa njia ya kielektroniki ambao watasaidia katika kupanga mikakati ya Jumuiya sambamba na kuhakikisha Chama cha Mapinduzi kinashinda kwa kishindo kikubwa katika uchaguzi mkuu wa nchi unaotarajiwa kufanyika mwaka 2025.
Mapema Makamo Mwenyekiti wa UWT Taifa Bi. Zainab Khamis Shomari amesema kuwa Mafunzo hayo waliopatiwa viongozi wa UWT yataleta mabadiliko chanya katika Utendaji kazi wa Jumuiya na Chama kwa Ujumla.
Amesema kuwa UWT wamejipanga kukipigania na kukilinda chama cha Mapinduzi kwa kuhakikisha kinafanya vizuri katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwisho wa mwaka huu na ule uchaguzi Mkuu wa nchi mwaka 2025 CCM inashinda na kuendelea kuiongoza nchi.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
28-10-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
28-10-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
28-10-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
28-10-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
28-10-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
28-10-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
28-10-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
28-10-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
28-10-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
28-10-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
28-10-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
28-10-2025
TAARIFA KWA UMMA
28-10-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
28-10-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
28-10-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
28-10-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
28-10-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
28-10-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
28-10-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
28-10-2025