SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imeeleza azma yake ya kutaka kusambaza umeme vijiji vyote vya Unguja na Pemba na kukuza maendeleo maeneo hayo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasema hayo Ikulu Zanzibar alipozungumza na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Tone Tinnes aliyekuja kujitambulisha.
Kwenye mazungumzo yao, wamegusia maeneo makuu manne ya ushirikiano uliopo baina pande mbili hizo za diplomasia ikiwemo Sekta ya Umeme, Mafuta na Gesi, Afya na Mazingira.
Kuhusu umeme Rais Dk. Mwinyi alimueleza Balozi, Tinnes kuangalia uwezekano wa kuongeza Ushirikiano uliopo baina ya Norway na Tanzania ikiwemo Zanzibar hasa kusambaza umeme vijijini ili kuviendeleza vijiji hivyo.
Akizungumzia sekta ya Mafuta na Gesi, Rais Dk. Mwinyi ameikaribisha Norway kuangalia fursa za uwekezaji kwenye maeneo hayo.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi alimueleza Balozi Tinnes kuongeza ushirikiano kwenye sekta ya Afya kupitia hospitali ya rufaa ya Mnazi Mmoja kwa wataalamu wa magonjwa ya moyo.
Akigusia suala za Mazingira Rais Dk. Mwinyi alieleza Zanzibar na Norway zimekua na ushirikinao mzuri kwenye maeneo hayo, sambamba na kuwawezesha na kuwaendeleza wanawake wa Zanzibar.
Dk. Mwinyi pia alimueleza Balozi huyo, kuangalia uwezakano wa kuwaendeleza wakulima wa mwani wa Zanzibar kupitia sekta ya Uchumi wa Buluu.
Alisema, Uchumi wa Buluu ni Sera kuu ya Zanzibar ya kukuza Uchumi wake ikifuatiwa na Utalii unaochangia asilimia 30 ya pato la taifa.
Naye, Balozi Tinnes alimuhakikishia Rais Dk. Mwinyi ushirikiano mzuri uliopo baina ya Ubalozi huo na Shirika la Umeme, Zanzibar (ZECO) kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati ya kukuza huduma za umeme kwa visiwa vya Zanzibar.
Balozi Tinnes alisema, ZECO na Ubalozi wa Norway nchini umefikia mazungumzo mazuri kwenye kuimarisha ushirikiano wao kupitia miradi mbalimbali ya Shirika hilo.
Kuhusu Sekta ya Afya, Balozi Tinnes alimueleza Rais Dk. Mwinyi ushirikino uliopo baina ya hospitali ya Mnazi Mmoja na Hospitali kuu ya Norway kuwa pande mbili hizo zinashirikiana kubadilishana uzoefu na kusaidiana wataalamu kwa maeneo tofauti.
Balozi Tinnes pia alisifu ushirikiano mzuri uliopo baina ya Taasisi za kodi za Tanzania ikiwemo Mamlaka ya Mapato Zanzibar, (ZRA) na taasisi ya kodi ya Norway, alisema Tanzania na Norway zinashirikiano kwa kubadilisha uzoefu na utaalamu wa maeneo hayo.
Pia Balozi huyo, alipongeza hatua kubwa ya Maendeleo iliyofikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na kupongeza miaka 60 ya ushirikiano wa diplomasia uliopo baina ya Tanzania na Norway uliotengeneza historia muhimu kwa jamii za pande zote mbili za ushirikiano kiuchumi na jamii.
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
09-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
09-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
09-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
09-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
09-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
09-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
09-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
09-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
09-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
09-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
09-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
09-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
09-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
09-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
09-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
09-12-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
09-12-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
09-12-2025