MAKAMO WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR MHE HEMED SULEIMAN ABDULLA AKIKAGUA UWANJA WA MICHEZO WA AMAANI MJINI ZANZIBAR
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla amesema kukamilika kwa Uwanja wa Michezo wa Amaani utatoa nafasi kwa Nchi mbali mbali Dunia kuweza kuutumia Uwanja huo utakaokuwa Uwanja wa kisasa uliokidhi Viwango vyote vya Kimataifa.
Ameyasema hayo alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendelea ya Ujenzi wa Kiwanja hicho uliopo katika hatua za mwisho kuweza kukamika.
Mhe Hemed amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dkt Hussen Ali Mwinyi kwa maono yake makubwa na nia thabiti ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Zanzibar kwa kuamua kuujenga upya Uwanja wa Amaani ili kuwawezesha wanamichezo wa Zanzibar na nje ya Zanzibar kucheza katika viwanja vyenye mandhari nzuri na hadhi ya Kimataifa.
Aidha Mhe. Makamu wa Pili wa Rais amesema kuwa Serikali inaimani kubwa na kampuni ya ORKUN inayojenga Uwanja huo na kuutaka uongozi wa kampuni hio kukamilisha ujenzi kwa wakati na kiwango kilichokusudiwa kwa maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
Amewataka wakandarasi na Mshuri elekezi wa Mradi huo kuongeza kasi ya ujenzi kwa kufanya kazi Usiku na Mchana na kwa uwaminifu mkubwa ili Ujenzi huo ukamilike kwa wakati na kwa kiwango kilichokusudiwa kwa maslahi ya vizazi vya sasa na vya baadae.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Ujenzi wa Uwanja huo ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi inayowataka Viongozi kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora zinazoendana na wakati ikiwemo michezo .
Sambamba na hayo Mhe Hemed amesema Sherehe za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar zinatarajiwa kufanyika katika Uwanja wa Amani kama alivyoahidi Mhe Rais wa Zanzibar Dkt Hussen Ali Mwinyi ili kutoa fursa kwa wanachi wengi kuweza kushiriki katika sherehe hizo pamoja na kujionea kile kilichofanywa na serikali ya awamu ya Nane (8).
Amewataka waandishi wa habari kutangaza mazuri na maendeleo yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya Nane (8) inayoongozwa na Rais Dkt Hussen Ali Mwinyi ambayo imedhamiria kuwaletea maendeleo endelevu wananchi wake.
Nae Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Bi. Fatma Hamad Rajab amesema Uwanja wa Amaani umejengwa kwa kufuata Vigezo vya Kimataifa na matakwa ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) ambao unatarajiwa kuchukuwa watazamaji elfu kumi na Sita (16,000) na kutoa fursa kwa Timu za ndani na nje ya nchi kuutumia Uwanja huo.
Amefahamisha kuwa Uwanja wa Amaani unajumuuisha Viwanja vya mpira wa miguu vya kisasa, uwanja wa Netball, Basket ball, Handball, Ukumbi wa Judo, Indows Game na Hoteli ambayo itasaidia kutoa huduma ya makaazi ya wageni watakaotoka nje ya Zanzibar.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Idrisa Kitwana Mustafa amesema Serikali ya Mkoa itahakikisha inatembelea mara kwa mara katika uwanja huo na kuhakikisha amani inatawala katika kiwanja hicho ambacho Serikali imewekeza fedha nyingi kwa maslahi ya Taifa.
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
04-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
04-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
04-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
04-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
04-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
04-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
04-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
04-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
04-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
04-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
04-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
04-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
04-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
04-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
04-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
04-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
04-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
04-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
04-03-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
04-03-2026