DR MWINYI AZIONYA TAASISI ZA SEREKALI ZINAZOKWEPA MATUMIZI YA MABADILIKO YA MIFUMO YA KISASA KWENYE UTENDAJI WAO
Alisema, kuna baadhi ya taasisi zinakiuka matumizi na miongozo ya mifumo iliyowekwa kisheria kwa utekelezaji na utendaji wa kazi zao, jambo alilolikataza mara moja kwani linakwamisha mipango na malengo ya Serikali. Dk. Mwinyi aliyasema hayo ukumbi wa Golden Tulip, Uwanja wa ndege Mkoa wa Mjini Magharibi kwenye uzinduzi wa Mkakati wa Kidijitali wa Serikali na Mfumo wa kitaifa wa Bajeti na Matumizi Serikalini (BAMAS). Aliwaagiza viongozi wa taasisi hizo wakiwemo Makatibu wakuu na wakuu wa taasisi
wanazozisimamia kuhakikisha wanapokea na kutumia mifumo ipasavyo kwa lengo la kujenga na kuimarisha miundombinu ya TEHAMA, sheria, miongozo, pamoja na taasisi zilizopewa majukumu ya kusimamia masuala hayo. “Nawaagiza viongozi wote wa Wizara, Idara, Taasisi za Serikali zote ikiwemo Mashirika na Taasisi za Kodi, Serikali Kuu na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kulisimamia agizo hili mara moja.” Aliagiza Rais Dk. Mwinyi.
Dk, Mwinyi alisema, Serikali itapunguza hujuma zinazofanywa na wachache kwa kutumia hati na nyaraka za kughushi na kuongeza mifumo imara, itatoa taarifa zilizotibitishwa kidijitali. Aliwaagiza Wakala wa Serikali Mtandao kupitia Ofisi ya Rais - Katiba, Sheria,
Utumishi na Utawala Bora kushirikiana na Ofisi ya Rais - Fedha na Mipango, kutoa elimu kwa taasisi zote za Serikali na wananchi juu ya mkakati wa pamoja na matumizi ya Mifumo mipya ya serikali inayoendelea kuzinduliwa. Alieleza, mfumo huo pia utaimarisha sekta muhimu za kiuchumi, uwekezaji na ukusanyaji wa mapato nchini kwa kuzingatia mbinu na mikakati ya kuimarisha na kuendeleza sekta za utalii, uchumi wa buluu, kuharakisha utoaji wa huduma bora za Jamii, ikiwemo bima ya afya, kuimarisha biashara hasa kwa raia wageni hawatolazimika kufika Ofisi za Serikali kufanya miamala au usajili wa biashara na kampuni zao badala yake popote walipo watafanya hivyo kwa muda mfupi kupitia njia za kidijitali.
Pia Rais Dk. Mwinyi aliongeza mfumo itarahisisha shughuli za usajili wa wanafunzi kwenye Skuli na vyuo vikuu, usajili wa ndoa, vizazi na vifo. Mfumo wa BAMAS pia umeondoa changamoto za mifumo inayoendelea kutumika
sasa ya ukusanyaji mapato (Isidore) na Mfumo wa Matumizi (Epicor) na kueleza kwamba BAMAS umeleta uwazi kwenye Bajeti na Matumizi Serikalini kwa kuwezesha Mifumo yote ya Malipo na Matumizi ya Fedha za Serikali kusomana kwa haraka na kwa ufanisi. Alieleza matarajio yake kwa Mfumo wa BAMAS kwamba utaongeza nguvu ya udhibiti wa mali za Serikali, uwajibikaji kwa Watumishi na watendaji wa Umma na kuhakikisha fedha za Umma zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa, ili kuwaletea wananchi maendeleo. Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango, Dk. Saada Mkuya Salum, alisema Mfumo wa BAMAS utaongeza ufanisi na utoaji wa huduma bora za Serikali pia utaunganisha pamoja sehemu ya mapato na matumizi
ya Serikali. Naye, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria, Utumishi na Utawala Bora, aliiomba Serikali kuiongezea uwezo taasisi ya wa badala ya kuwa wakala kuwa
Mamlaka ili kuiongezea ufanisi na usimamiaji mzuri wa matumizi mtandao kwa taasisi zote za Serikali. Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala Serikali Mtandao Zanzibar, SaidiSeif Said alieleza kwa kipindi cha miaka miwili na nusu sasa wametengeneza na kusimamia mifumo 28 ukiwemo mfumo wa BAMAS na kueleza kwelekeo wa taasisi hiyo ni kuongeza kasi ya kutengeneza mifumo yenye nguvu zaidi ili kuongeza ufanisi wa kiutendaji kwa taasisi za Serikali.
Uzinduzi wa Mkakati wa Kidijitali wa Serikali na Mfumo wa Bajeti na Matumizi Serikalini (BAMAS) ulikwenda sambamba na kaulimbiu “Hatma yetu ipo viganjani mwetu”
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
27-10-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
27-10-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
27-10-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
27-10-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
27-10-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
27-10-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
27-10-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
27-10-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
27-10-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
27-10-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
27-10-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
27-10-2025
TAARIFA KWA UMMA
27-10-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
27-10-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
27-10-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
27-10-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
27-10-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
27-10-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
27-10-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
27-10-2025