MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
Naibu Katibu Mkuu CCM (Bara) Ndg. John Mongella Leo Tarehe 22 Juni, 2025 ameongoza Mazishi ya Aliyekuwa Kada wa CCM, Mobutu Malima aliyefariki Dunia Tarehe 15 Juni, 2025, Jijini Dodoma, kwa Maradhi ya Shinikizo la Damu, hadi umauti unamfika Marehemu Malima alikuwa Mtumishi wa CCM Makao Makuu jijini Dodoma, na katika utumishi wake alishika nyadhifa Mbalimbali ndani ya Chama ikiwa ni pamoja na kutumikia nafasi ya Katibu wa CCM katika Mikoa tofauti tofauti.
Katika Mazishi hayo Mongella aliambatana pia na Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Wajumbe wa Halmashauri Kuu, Wenyeviti wa Mikoa na Makatibu wa Mikoa Mbalimbali, pamoja na Wanachama wa CCM.
Mungu ametoa na Mungu Ametwaa Jina Lake Lihimidiwe