NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa, amewasihi Wananchi wa Jimbo la Kwahani kufanya maamuzi sahihi ya kumchagua mgombea aliyesimamishwa na CCM kwani ndiye mwenye uwezo wa kuendeleza utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 kwa vitendo.
Nasaha hizo amezitoa wakati akizindua kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo hilo katika Uwanja wa Tawi la CCM Sebleni Zanzibar.
Alisema CCM imejipanga kuhakikisha mgombea wake anashinda katika Uchaguzi huo ili kuendeleza maendeleo na ustawi wa jamii katika Jimbo hilo ambalo ni ngome ya CCM toka kuanzishwa kwa mfumo wa Vyama vingi vya siasa nchini.
Katika maelezo yake Dkt.Dimwa,amesema Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Mwinyi amefanya kazi kubwa na nzuri,hivyo anastahili kupewa Viongozi imara na makini wanaotokana na CCM ili wamsaidie kazi.
" Maendeleo ya Jimbo hili yatazidi kuimarika zaidi chini ya Viongozi wachapakazi,waadilifu na wachapakazi wanaojali utu na maisha ya Wananchi wote bila ubaguzi wa kisiasa,kikabila na kidini na kazi hiyo ataifanya kwa ufanisi mkubwa ndugu yetu Khamis Pele." alisisitiza Dkt.Dimwa.
Akizungumzia mafanikio ya CCM katika utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 uliofanyika katika Jimbo la Kwahani ikiwemo ujenzi wa Skuli ya kisasa ya ghorofa Shehia ya Muungano iliyogharimu zaidi ya Bilioni 6.1,ujenzi wa Soko la Kwahani uliogharimu kiasi cha zaidi ya milioni 500, wanufaika wa miradi wa TASAF ni 242 unaogharimu zaidi ya milioni 577.4 pamoja na utoaji wa Pencheni Jamii kwa Wazee 582.
Pia utekeleza wa Ilani ya CCM kwa upande wa Mbunge na Mwakilishi wameimarisha sekta za Elimu,afya,maji safi na Salama, ujenzi wa Ofisi za CCM ngazi zote,vikundi vya ujasirimali, ununuzi wa vifaa vya michezo na misaada ya Kijamii kwa Wananchi vilivyogharimu shilingi 467.8.
Kupitia Mkutano huo Dkt.Dimwa, alimkabidhi Ilani ya Uchaguzi Mgombea huyo Khamis Yussuf Mussa (Pele), na kumsisitiza kuwa ilani hiyo ndio mkataba kati ya wananchi na CCM hivyo akishinda kazi kubwa ya kuendeleza maendeleo kwa wananchi wa jimbo hilo.
Kampeni hizo za Uchaguzi huo zinafanyika kutokana na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Ahmada Yahya Abdul Wakil (Shaa) tarehe 8,April 2024 kwa maradhi ya shinikizo la damu, na Uchaguzi huo umepangwa kufanyika June 8, mwaka 2024.
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
27-03-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
27-03-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
27-03-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
27-03-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
27-03-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
27-03-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
27-03-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
27-03-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
27-03-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
27-03-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
27-03-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
27-03-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
27-03-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
27-03-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
27-03-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
27-03-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
27-03-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
27-03-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
27-03-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
27-03-2026