UDINI NI HATARI, KUCHOMA NGUO NI UTOTO
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amewahimiza Watanzania kuendelea kushirikiana na CCM, akisisitiza kuwa chama hicho kimeonyesha kwa vitendo uwezo wa kuongoza nchi na dhamira ya kuwahudumia wananchi wanyonge.
Dkt. Nchimbi alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Lamadi, Wilaya ya Busega na Kata ya Dutwa, wilayani Bariadi, mkoani Simiyu, kwa nyakati tofauti leo, tarehe 6 Oktoba 2024.
Hii ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika mkoa huo, ambapo alieleza kuwa CCM imekuwa ikiandaa viongozi wake kwa ufanisi.
“Kiongozi aliyeandaliwa vizuri hueleza mipango yake waziwazi anapopewa nafasi: ‘Nikitwaa madaraka, nitafanya moja, mbili, tatu.’ Lakini kiongozi ambaye hajakomaa, anapewa nafasi ya kuzungumza na kuanza kuhamasisha maandamano, kuchoma nguo, au kuzomea watu, hapo unajua bado hajakomaa na anahitaji muda wa kujifunza zaidi.”
“Katika CCM, hatuna viongozi wanaoshikilia madaraka kwa miaka 40. Viongozi wanachaguliwa, wanapungua, na wengine wanapewa nafasi. Ukiangalia baraza la kwanza la mawaziri la Tanganyika, leo hii hakuna hata mmoja aliyebakia kwenye baraza. Kila uongozi unaleta sura mpya. Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu wa miaka mitano iliyopita, leo hayupo. Hii ndiyo CCM.”
Balozi Nchimbi alisisitiza kuwa hii ndiyo sababu CCM kinaendelea kuwa chama chenye nguvu, kijana kuliko vyama vingine nchini, kwani uhai wa chama unategemea wanachama na viongozi wake.
“Huwezi kusikia mwanachama mkongwe wa CCM akishabikia udini au ukabila. Lakini kuna viongozi wa vyama vingine ambao wameonyesha kushabikia hayo kwa sababu hawana historia ya kuijenga nchi hii, wala hawajui maumivu ya watu wake. Wao hawaitazami nchi kwa mbali, ndiyo maana wanaweza kutoa matamshi bila kujali madhara yanayoweza kutokea,” aliongeza Balozi Nchimbi.
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
29-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
29-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
29-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
29-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
29-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
29-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
29-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
29-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
29-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
29-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
29-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
29-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
29-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
29-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
29-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
29-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
29-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
29-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
29-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
29-05-2026