KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, amewataka wanasiasa nchini kuwa wangwana na kufuata nyayo za Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui aliyekiri na kusifu kazi kubwa inayofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Mwinyi kwa kusimamia kwa ufanisi utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi CCM ya mwaka 2020/2025 katika sekta ya Afya nchini.
Kauli hiyo ameitoa katika mahojiano maalum huko Afisini kwake Kisiwandui Zanzibar, alisema kasi ya utendaji wa Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi katika kuimarisha sekta mbali mbali nchini hasa Wizara ya Afya imevuka malengo ya Ilani ya CCM.
Mbeto, alisema kitendo cha Waziri wa Afya Zanzibar ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo Nassor Mazrui jana katika ufunguzi na makabidhiano ya nyumba za wafanyakazi hospitali ya Abdulla Mzee Mkoa wa Kusini Pemba kukiri na kupongeza kasi ya utendaji wa Dk.Mwinyi ni uzalendo mkubwa unaotakiwa kuwa fundisho kwa wanasiasa wengine nchini kujitathimini kisiasa,kimaono na kifikra.
Alisema kitendo cha kiongozi huyo mkuu wa Chama cha upinzani nchini kujitokeza hadharani kusifu utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 katika Wizara ya Afya ni salamu za pekee kwa vyama vya upinzani nchini kuwa CCM itashinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu ujao.
Katika maelezo yake Mbeto, alifafanua kuwa Waziri huyo Mazrui alimsihi Dkt.Mwinyi aendelee kufanya kazi wala asijali maneno ya watu kwani utendaji wake unaonekana kwa wananchi.
"Chama Cha Mapinduzi Zanzibar tunaposema hatuna mbadala wa Dk.Mwinyi tunaimanisha kwani kazi tuliyopewa na wananchi ya kuleta maendeleo endelevu tayari imefanyika katika sekta mbalimbali tunachosubiri ni wananchi kujaza visanduku vya kura nyingi za ndio kwa nafasi za Rais,Wabunge,Wawakilishi na Madiwani wa CCM.
Kuona kiongozi wa timu ya mkakati ya Chama cha ACT-Wazalendo Nassor Mazrui anamsifu Rais Dk.Mwinyi sio jambo dogo kuna kazi kubwa imefanyika mpaka kuweka mbele uzalendo badala ya kubeza na kukosoa.", alisema Mbeto.
Mbeto,alisema katika sekta ya afya Serikali imejenga vituo vya afya vya kisasa zaidi ya 10 kila wilaya pia hospitali kubwa ya Mkoa yenye vifaa tiba vya kisasa nchini.
Alifafanua kuwa serikali ya awamu ya nane ya Zanzibar chini ya uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Mwinyi, imetekeleza mambo mengi ya maendeleo ikiwemo kufikisha huduma ya umeme kwa gharama nafuu,ujenzi wa barabara za kisasa,ujenzi wa skuli,kuongeza pencheni kwa wazee,kuongeza mishahara kwa watumishi wa umma pamoja na kuimarisha miundombinu ya sekta binafsi.
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
31-05-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
31-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
31-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
31-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
31-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
31-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
31-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
31-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
31-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
31-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
31-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
31-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
31-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
31-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
31-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
31-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
31-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
31-05-2026