RAIS DKT. SAMIA ACHANGIA SH. MILIONI 50 KUMUENZI PADRI SHIRIMA
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa shilingi milioni 50 kwa ajili ya maendeleo ya Shule ya Sekondari ya Seminari Uru, mkoani Kilimanjaro.
Mchango huo umetolewa ili kuweka alama ya kumbukumbu ya kumuenzi marehemu Padri Canute Mkwe Shirima AJ, aliyewahi kuwa Baba Gombera wa shule hiyo, mojawapo ya seminari maarufu nchini.
Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, alitangaza mchango huo kwa niaba ya Rais Dkt. Samia alipokuwa akitoa salaam za pole na rambirambi katika ibada ya mazishi ya Padri Shirima, iliyofanyika Seminari ya Uru, Alhamisi, Machi 20, 2025.
“Haya yote niliyoyasema hapa kumhusu Baba Gombera mstaafu Padri Canute Shirima, alivyokuwa mlezi mzuri akifundisha nidhamu na uwajibikaji, nilimwambia Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
“Nilimtaarifu kuwa nakatisha ziara ili kuhudhuria mazishi haya. Mheshimiwa Rais akaniambia anatoa shilingi milioni 50 kwa Seminari ya Uru ili mtengeneze jambo lolote litakaloenzi heshima ya Padri Shirima,” alisema Balozi Nchimbi.
Akizungumzia marehemu Padri Shirima, Dkt. Nchimbi, ambaye pia aliwahi kuwa mwanafunzi wa seminari hiyo, alisema alikuwa mwalimu mahiri aliyesisitiza nidhamu na uwajibikaji kwa wanafunzi wake.
Aliongeza kuwa uongozi wa Padri Shirima ulisaidia Seminari ya Uru kupata sifa kubwa kwa kutoa wahitimu waliodhihirisha uwezo mkubwa katika nyanja mbalimbali.
“Tunawashukuru sana wazazi wa Padri Shirima kwa malezi mazuri waliyompa, ambayo nasi tuliyapata kupitia yeye. Asanteni sana Mapadri Watume wa Yesu Kristo na mapadri wote mliopo. Asante sana Baba Askofu Minde kwa heshima hii ya kuja kuongoza ibada ya kumuaga mwalimu wetu,” alisema Balozi Nchimbi.
Akiongoza ibada hiyo, Askofu wa Jimbo Katoliki la Moshi, Mhashamu Askofu Rudovick Joseph Minde ALCP/OSS, alisema marehemu Padri Shirima alikuwa zawadi ya Mungu kwa jamii aliyowatumikia.
“Kwa namna alivyoshuhudiwa hapa na umati huu uliokusanyika, mmeona na kusikia jinsi alivyolea watu wakubwa sasa, wakiwemo maaskofu, mapadri, viongozi wa juu serikalini, na hata tumepata salaam kutoka Ofisi ya Rais… Padri Canute alikuwa zawadi ya Mungu kwetu,” alisema Askofu Minde.
Padri Canute Mkwe Shirima, wa Shirika la Watume wa Yesu, ambaye alifariki akiwa katika utume nchini Afrika Kusini, alizikwa kwa heshima zote za Kanisa Katoliki katika makaburi ya Shule ya Sekondari ya Seminari Uru, Moshi, Kilimanjaro.
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
28-02-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
28-02-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
28-02-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
28-02-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
28-02-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
28-02-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
28-02-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
28-02-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
28-02-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
28-02-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
28-02-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
28-02-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
28-02-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
28-02-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
28-02-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
28-02-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
28-02-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
28-02-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
28-02-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
28-02-2026