BALOZI DKT. NCHIMBI AZURU KABURI LA HAYATI JOHN KOMBA
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, Jumapili, Aprili 21, 2024, amezuru kaburi la Hayati Kepteni (mst) John Damiano Komba na kutoa heshima zake kwenye kaburi hilo kwa kuweka shada la maua.
Dkt. Nchimbi ambaye ameambatana na Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu. Amos Makalla, Katibu wa NEC - Oganaizesheni wa CCM Taifa Ndugu. Issa Haji Gavu pamoja na Katibu wa NEC- Uchumi na Fedha Ndugu Dk. Frank George Haule Hawassi, pia alipata wasaa wa kuwasalimia na kuwapatia pole familia, ndugu, jamaa, marafiki na wananchi wa Kijiji cha Lituhi, alipozikwa Kepteni Komba.
Hayati Komba, ambaye alikuwa mhamasishaji mkuu wa CCM, akiwa pia amefanya kazi kubwa ya nchi, kupitia kazi za sanaa, na aliwahi kuwa Mbunge wa Majimbo ya Mbinga Magharibi na Nyasa, kwa nyakati tofauti, kwa tiketi ya CCM, alifariki dunia mwaka 2015 tarehe 28 mwezi Februari.
Akiwa hapo Lituhi, Dkt. Nchimbi, amekutana na familia na wananchi wa maeneo ya karibu waliojitokeza kuungana nae katika kuzuru kaburi la Komba na kumuombea apumzike kwa amani.
”Kwa niaba ya viongozi wenzangu na wanachama wote wa CCM, tumekuja mahali hapa kuona kaburi la aliyekuwa mkuu wa vikosi vya sanaa vya CCM na ni kwa sababu ya kuthamini na kutambua mchango mkubwa katika kushiriki na kuandaa Taifa, vita ya kuitetea Tanzania dhidi ya Uganda, kutangaza na kutoa elimu juu ya ugonjwa wa Ukimwi, kuimarisha sanaa kwa mziki wa jadi na wa kisasa pamoja na mengine mengi yenye msingi imara kwa Taifa letu. CCM itaendelea kuthamini na kuhakikisha aliyoyaanzisha hayati Kepteni Komba hayapotei bure,” amesema Dkt. Nchimbi.
Naye, Dkt. George John Komba kwa niaba ya familia ya marehemu Komba, amesema;
“Tunatoa shukrani kwa CCM kuanzia kwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na viongozi wote wa taifa, mkoa, wilaya , kata, matawi, mashina na wajumbe wote kwa kuedelea kukumbuka kazi ya hayati Kepteni Komba ambaye kwetu ni Baba lakini kwenu ni askari jasiri ambaye amepigana na kushiriki katika kampeni za CCM kupata ushindi wa kishindo katika awamu zote.
”Familia tunawahakikishia tutaendelea kuwa wananchama waadilifu wa CCM sababu mafanikio yetu sote ni yanatokana na CCM na alituachia urithi kwa kusema isitokee hata mmoja akahama kwenda upande tofauti na CCM nasi tunaahidi kukienzi na kuwa wanachama wa hai.”
ποΈ21 Aprili, 2024
πLituhi - Ruvuma
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
28-02-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
28-02-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
28-02-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
28-02-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
28-02-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
28-02-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
28-02-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
28-02-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
28-02-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
28-02-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
28-02-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
28-02-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
28-02-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
28-02-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
28-02-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
28-02-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
28-02-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
28-02-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
28-02-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
28-02-2026