SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR IMELISHUKURU SHIRIKA LA MAENDELEO LAUMOJA WA MATAIFA (UNDP) KWA JITIHADA ZAKE ZA KUENDELEA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI KUPITIA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema UNDP limekua msaada mkubwa kwa SMZ hasa kwa kuendelea kushirikiana kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kuiongezea nguvu na kuiwezesha kifedha Taasisi ya Ufuatiliaji na Usimamizi Utendaji Kazi Serikalini (PDB), Zanzibar ili kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
Dk. Mwinyi amesema hayo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika hilo, nchini Shigeki Komatsubara aliefika kumtembelea. Alisema, SMZ na UNDP zimekua na ushirikiano wa karibu kwa miaka mingi na wamekua wakiungamkono Serikali kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo.
Rais Dk. Mwinyi alimueleza mgeni wake huyo, Sera kuu ya Uchumi wa Zanzibar ni Uchumi wa Buluu, hivyo alimueleza kuangalia fursa zaidi za kuungamkono eneo hilo pamoja na Sekta ya Utalii. Dk. Mwinyi pia alilipongeza Shirika la UNDP kwa juhudi zake za kusaidia vyombo vya Sheria nchini ikiwemo Bunge kwa Tanzania Bara, Baraza la Wawakilishi na Mahakama kwa kuzijengea uwezo taasisi hizo.
Naye, Bw. Shigeki Komatsubara, alimuahidi Rais Dk. Mwinyi kwamba UNDP itaendeleza Ushirikiano kwa kuendelea kufanyakazi pamoja na SMZ kupitia Sekta ya Uchumi wa Buluu pamoja na kuendelea kuiungamkono PDB kupitia miradi mbalimbali ya Serikali.
Akizungumza baada ya hafla hiyo, Naibu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Ufuatiliaji na Usimamizi Utendaji Kazi Serikalini (PDB) Zanzibar, Dk. Josephine Rogate Kimaro alilishukuru Shirika la UNDP kwa ushirikiano mkubwa wanaoipatia PDB ikiwemo kuwajengea uwezo kwenye utendajikazi wao.
Alisema, UNDP limekua likiungamkono masuala mbalimbali ya maaendeleo ya taasisi hiyo hasa kwenye usimamizi na utekelezaji wa miradi ya kimkakati na kuweka mifumo ya utekeleza wa miradi ya vipaombele pamoja na kuisaidia taasisi hiyo kwenye ushajihishaji wa rasilimali zake.
Shirika la UNDP linatekeleza miradi sita barani Afrika, ikiwemo mitatu kwa Tanzania ambapo Zanzibar wanashirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutekeleza miradi ya kupambana na matukio ya Uhalifu Zanzibar kwa
kusirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka chini ya ufadhili wa Serikali ya Uingereza na Umoja wa Ulaya (EU).
Mradi mwengine unaotekelezwa na UNDP ni uwezeshaji kwenye masuala ya utawala wa kisheria ambapo mradi unaangazia juu ya haki na wajibu kwenye masuala ya jinsia ikiwemo masuala ya wanawake na watoto.
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
07-11-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
07-11-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
07-11-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
07-11-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
07-11-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
07-11-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
07-11-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
07-11-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
07-11-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
07-11-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
07-11-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
07-11-2025
TAARIFA KWA UMMA
07-11-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
07-11-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
07-11-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
07-11-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
07-11-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
07-11-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
07-11-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
07-11-2025