Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema atahakikisha Chama Cha Mapinduzi kuwa na uchumi wa uhakika utaowezesha watumishi kulipwa posho hususan mabalozi.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema atahakikisha Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar kina kuwa na uchumi wa uhakika ambao utawawezesha watumishi kulipwa posho hususan mabalozi.
Kauli hiyo ameitoa jana wakati akizungumza na mabalozi, wajumbe wa Halmashauri kuu za, Majimbo, wilaya na Mkoa wa Kaskazini Pemba katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi uliopo Wete. Alisema endapo rasilimali zilizopo ndani ya chama zikiwekezwa vizuri CCM itajiendesha bila wasi wasi wowote. Pia, alisema kupitia Uwekezaji huo wa rasilimali hizo itarahisisha chama kuwalipa posho watumishi wake ili waweze kufanya kazi vizuri. "Ninatambua kuwa watendaji wengine katika ngazi ya Mkoa na wilaya wanalipwa lakini haitoshi lazima twende chini zaidi twende jimbo,wadi,matawi na hatimaye tuwafikie mabalozi,"alisema
Alisema hatua hiyo itasaidia kufanya kazi vizuri na kwamba katika jambo hilo amewaomba wanachama wa CCM kumpa ushirikiano ili kujenga uchumi mzuri wa chama. Rais Dk.Mwinyi alisema kuna kila sababu ya kuijenga CCM kiuchumi kutokana na kuwa shughuli nyingi za kisiasa zinahitaji fedha. "Ili kazi zote za chama zifanyike Kwa maana tuwe na ofisi nzuri na vitendea kazi ikiwemo vyombo vya usafiri lazima tujenge uchumi wetu wa chama chetu,"alisema. Alisema katika ziara ambazo amezifanya Kwa Unguja na Pemba amejionea miradi mingi ya chama na kwamba endapo itatumika vizuri kitaweza kujiendesha chenyewe. "Ahadi yangu kwenu wanachama wa Mapinduzi nitatafuta mbinu za kuziendesha rasilimali zetu za chama vizuri tupate mapato mazuri tujenge ofisi zetu nzuri,tujenge ukumbi wa mikutano, tuwe na vyombo vya usafiri,"alisema
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Mohammed Said Mohammed 'Dimwa' alisema maagizo yote aliyoyatoa Rais Dk.Mwinyi ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar chama kishaanza kufanyiwa kazi. "Tushaanza kuyafanyia kazi ikiwemo kutoa mafunzo Kwa watendaji Kwa upande wa Unguja ambapo ikitoka huko tutafanya Pemba,"alisema. Alisema agizo lingine la Rais Dk.Mwinyi ambapo limeanza kutekelezwa ni ugawaji wa vitambulisho kwa mabalozi. "Unguja tushaanza kuwapatia vitambulisho mabalozi hao na kila balozi atapata kitambulisho chake pamoja na Mambo yetu yataanza kuratibu,"alisema
Naye Katibu wa Idara ya Siasa,Uhusiano na Kimataifa CCM, Mbarouk Nassoro Mbarouk alisema katika kipindi cha miaka miwili cha Rais Dk.Mwinyi amekuwa akitangaza kipaumbele chake ni serikali ya umoja wa kitaifa. "Sasa hivi tunaona matunda yake ya kuwepo kwa hali ya amani ambapo wawekezaji wengi wamekuwa wakivutiwa kuja kuwekeza hapa Zanzibar,"alisema. Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba Mberwa Hamad Mberwa alisema Kaskazini Pemba ipo salama na kwamba chama na Serikali kinashirikiana kwa karibu. "Tumefanya uchaguzi kwa ngazi ya Uwakikishi na Ubunge pamoja na chama ambapo katika uchaguzi huo ulijitokeza baadhi ya changamoto na baada ya uchaguzi huo kwa sasa hali nzuri na tumekuwa na umoja ndani ya chama chetu ,"alisema
Mwenyekiti huyo alisema chama kina unga mkono jitihada za serikali ya awamu ya nane katika azma yake ya kujenga bandari ya Wete.
Akimkabidhi kadi ya CUF kwa Rais Dk.Mwinyi, Mbarouk Ali Mbarouk ambaye ni Katibu wa Jimbo la Tumbe alisema amehamia CCM kwa kutokana na kazi nzuri zinazofanywa na Serikali. "Baada ya kukaa na Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana(UVCCM) wilaya ya Micheweni Shakira Mohamed Hija nikahamasika na baadaye nikawashawishi vijana zaidi 300 Jimbo la Tumbe kujiunga na CCM na Leo wapo hapa mbele,"alisema. Alisema kutokana na utendaji wa serikali ya awamu ya nane hatoishia hapo na badala ya atahakikisha anawahamisha wazee kujiunga na CCM. "Kwa ridhaa yangu wala sijalazimisha kuhamia CCM nina kabidhi kadi yangu hii ya CUF kwako Mheshimiwa Makamu Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Rais wa Zanzibar Dk.Mwinyi,"alisema
Nae Kombo Mkadamu Khatibu ambaye ni mwanachama wa CUF alisema kwa upande wake anampongeza Rais Dk.Mwinyi Kwa uchapakazi wake. "Hakuna chama chochote cha siasa hapa Zanzibar kitakacholeta kiongozi mcha Mungu kama Rais Dk.Mwinyi kutoka CCM,"alisema . Alisema kutokana na maendeleo yanayoonekana kupitia serikali ya awamu ya nane yeye na watoto wake wanahamia CCM.
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
31-05-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
31-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
31-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
31-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
31-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
31-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
31-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
31-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
31-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
31-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
31-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
31-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
31-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
31-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
31-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
31-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
31-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
31-05-2026