CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar champongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi kwa azma yake ya kuifungua Pemba kiuchumi
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi kwa azma yake ya kuifungua kiuchumi kisiwa cha Pemba.
Kauli hiyo ameitoa Katibu wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Idara ya Itikadi na Uenezi,Zanzibar Khamis Mbeto Khamis kwenye mkutano wa Rais Dk.Mwinyi ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Halmashauri kuu za Majimbo,wilaya na mkoa wa Kusini Pemba.
Alisema serikali ya awamu ya nane inatarajia kujenga uwanja wa kisasa wa ndege wa Pemba wenye urefu wa mita 2500 katika njia ya kurukia ndege. Katibu huyo alisema mbali na hilo serikali inayoongozwa na Rais Dk.Mwinyi tayari imeshafikisha huduma za umeme kwenye vijiji 65 ambapo kati ya vijiji hivyo vijiji 22 ni kutoka kisiwa cha Pemba. Alisema bajeti ijayo ya serikali itakwenda kukamilisha vijiji vingine vilivyobakia katika kufikisha huduma za umeme."Mheshimiwa Rais katika huduma za maji safi na salama takribani shehia 470 kwa Unguja na Pemba zimefikiwa na huduma hiyo muhimu,"alisema
Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Kusini Pemba Matar Zahor alisema eneo la sekta ya elimu serikali inayoongozwa na Rais Dk.Mwinyi katika kipindi hiki imetengeneza madarasa 158 kwenye mkoa wake ambayopo ndani yake kuna shule tatu za ghorofa na tayari zimekwishaanza kutumika. "Lakini pia mchakato unaendelea ya kuyajenga madarasa mengine kazi imeanza shule ya Ole,Michakaini na tunatarajia kupata shule ya ghorofa kwenye eneo la kengeja na Wesha,"alisema
Alisema kwa upande wa ajira mkoa wa kusini Pemba imepata ajira mpya 981 za walimu na kwamba bado kuna ajira 500 ambazo zinatarajiwa kupatikana kupitia eneo hilo la sekta ya elimu baada ya kukamilika kwa mchakato wa kuajiri.
"Katika eneo la miundombinu ya barabara mkoa wetu tunaendelea vizuri tumekamilisha hivi karibuni barabara ya Kijangwani Birikau yenye urefu wa kilomita 4.2 kwa kiwango cha lami na barabara ya Kipapo Mgelema yenye urefu wa kilomita 6.4 imeanza kuwekwa lami,"alisema
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
29-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
29-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
29-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
29-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
29-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
29-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
29-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
29-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
29-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
29-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
29-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
29-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
29-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
29-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
29-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
29-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
29-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
29-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
29-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
29-05-2026