KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis,amesema Chama Cha Mapinduzi kitaendelea kuwasimamia Viongozi wa Majimbo hasa Wabunge na Wawakilishi watekeleze kwa ufanisi ahadi walizotoa kwa Wananchi kupitia Uchaguzi Mkuu uliopita.
Hayo ameyasema wakati akikabidhi vitendea kazi vikiwemo mitungi ya Gesi na Pikipiki kwa Viongozi wa jimbo la Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo hilo Mhe.Profesa Makame Mbarawa Mnyaa.
Amesema CCM ipo kwa ajili ya kusimamia maslahi na haki za wananchi kwa kuhakikisha kila kiongozi aliyepewa dhamana ya kuwawakilisha Wananchi katika Vyombo vya maamuzi anatekeleza wajibu wake kwa wananchi.
Katika maelezo yake Mbeto,amefafanua kuwa CCM katika Uchaguzi Mkuu ujao CCM itatoa kipaumbele kwa Viongozi wanaofanya kazi kwa ufanisi na waliokuwa karibu na Wananchi wao.
"Nakupongeza sana Prof.Mbarawa umefanya kazi kubwa ya kutekeleza Ilani ya CCM kwani changamoto kubwa iliyokuwa ikiwakabili Viongozi na Watendaji wengi wa ngazi za Matawi hadi Majimbo ni ukosefu wa usafiri wa kutoka eneo moja kwenda jingine,lakini kwa busara zako leo umewapatia Pikipiki na akina mama kuwapa Gesi salama kwa ajili ya ulinzi wa miundombinu ya mazingira", alisema Mbeto.
Kupitia hafla hiyo ya makabidhiano ya vifaa hivyo Mbeto,aliwataka Viongozi na Wanachama kuhamasisha wananchi kujiunga na CCM kwa wingi.
Akizungumzia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 amesema tayari imetekelezwa kwa zaidi ya asilimia 98 kwa kipindi cha miaka mitatu ya Uongozi wa Rais Dk.Mwinyi.
Pamoja na hayo Mbeto,alimpongeza Mbunge huyo Prof.Mbarawa kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwaletea wananchi maendeleo katika sekta za maji safi na salama,miundombinu ya usafiri,afya,elimu na vikundi vya ujasiriamali na kwamba viongozi wengine waige mfano huo katika kuharakisha maendeleo endelevu ya majimbo.
Naye Mbunge wa Jimbo la Mkoani,Prof.Makame Mbarawa,Amewapongeza wanachama wa CCM kwa kazi kubwa wanayofanya ya kukitumikia Chama kwa kujitoleo.
Alisema leongo la kutoa mitungi ya Gesi ni kuunga mkono kampeni ya mazingira za kuhamasisha matumizi salama ya Gesi majumbani badala ya kuni na mkaa.
Aidha,amesema dhamira ya kutoa Pikipiki kwa Watendaji mbali mbali wa Chama ndani ya Mkoa huo ni kuwarahisishia huduma za usafiri wakati wa utekelezaji wa Majukumu yao ya kila siku.
Katika hafla hiyo Mbunge huyo wa Jimbo la Mikoani ametoa Pikipiki 20 zenye thamani ya shilingi milioni 64 pamoja na mitungi ya Gesi 200 kwa ajili ya Wananchi wa Jimbo hilo.
𝐌𝐖𝐄𝐍𝐄𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐀𝐀𝐍𝐙𝐀 𝐙𝐈𝐀𝐑𝐀 𝐖𝐈𝐋𝐀𝐘𝐀 𝐘𝐀 𝐇𝐀𝐈 𝐌𝐊𝐎𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
𝐍𝐈 𝐌𝐔𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐇𝐀𝐈-𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎 𝐒𝐀𝐒𝐀
31-05-2026
𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐏𝐀 𝐁𝐀𝐉𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐊𝐀𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐒𝐈𝐇𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐔𝐋𝐄𝐌𝐀𝐕𝐔 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐆𝐔𝐔
31-05-2026
MAWENZI YAVUNJA REKODI: MITUNGI 3,313 YA OKSIJENI YAZALISHWA KWA MIEZI 6, ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 126 ZAOKOLEWA!
31-05-2026
MAFURIKO YA WANANCHI WA SIHA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA HADHARA
31-05-2026
MAPOKEZI YA KATIBU MWENEZI WA CCM NDUGU KENANI L KIHONGOSI MKOANI KILIMANJARO
31-05-2026
🔰 𝐊𝐈𝐇𝐎𝐍𝐆𝐎𝐒𝐈 𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐎 𝐊𝐈𝐋𝐈𝐌𝐀𝐍𝐉𝐀𝐑𝐎
31-05-2026
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
31-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
31-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
31-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
31-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
31-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
31-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
31-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
31-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
31-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
31-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
31-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
31-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
31-05-2026