CCM CHINI YA MWENYEKITI DKT. SAMIA IMEENDELEA KUTUAMINI VIJANA, TUCHAPE KAZI TUSIMUANGUSHE - CDE. JOKATE
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Komredi. Jokate Mwegelo, amewataka vijana wote wanaoaminiwa na kupewa nafasi za uongozi ndani ya chama au serikali kufanya kazi kwa bidii na kwa ubunifu wa hali ya juu kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla.
Komredii Jokate ameyasema hayo wakat akizungumza kwenye kikao na viongozi wa Chama na Jumuiya ya UVCCM Mkoa wa Iringa mara baada ya kuwasili na kupokea taarifa ya kazi ya UVCCM mkoani humo.
"Yatupasa wakati wote kutoa shukrani kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinachoongozwa na Mwenyekiti na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kutuamini vijana hususani vijana wa kike na kutuamini katika kutupa nafasi za uongozi ndani ya chama na serikali yetu hivyo ni wajibu na ulazima kufanya kazi kwa bidii na ubunifu kwa manufaa ya chama, serikali na Taifa kwa ujumla"
Akiendelea kuzungumza na viongozi hao, Komredi Jokate amesisitiza juu ya Ushirikano katika kufanya kazi.
"Kikubwa kwetu ni ushirikiano wa kutosha na kufanya kazi kubwa kulingana na wajibu wetu katika kuhakikisha vijana wanapata fursa mbalimbali hususani kuwainua kiuchumi, kuendelea kuwasemea vema viongozi wetu wa chama na serikali na kuhakikisha CCM inaendelea kushika dola."
Aidha, Komredi Jokate amesema lengo kubwa la kuwasili mkoani Iringa ni mpango mkakati wa kuinua kituo cha Ihemi kuwa chachu na fursa zaidi kwa vijana.
"Tumekuja hapa kuangalia fursa za kuendeleza kituo chetu cha Ihemi na hivi karibuni tutakuwa na mafunzo kwa viongozi wetu wa wilaya nchi nzima."
"Tunataka kuimarisha kituo cha Ihemi na kwa namna tulivyojipanga tuna hakika tutaweza kufikia adhma hiyo."
"Niwasihi vijana wenzangu wa CCM , chama chetu kina namna na utartibu wake wa kuwasilisha majambo yetu na changamoto zetu hata za baina yetu ya sisi kwa sisi kupitia vikao na si kutumia njia zingine ambazo ni sawa na kuwa faida wapinzani kupata la kusemea, tuwe wazalendo, tupende chama na nchi yetu na tuwe na utulivu."
π21 Juni, 2024
πMkoani Iringa
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
30-12-2025
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
30-12-2025
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
30-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
30-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
30-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
30-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
30-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
30-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
30-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
30-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
30-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
30-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
30-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
30-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
30-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
30-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
30-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
30-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
30-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
30-12-2025