MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR ALHAJJ HEMED SULEIMAN ABDULLA AMEWATAKA WAZAZI NA WALEZI KUWASIMAMIA VIJANA WAO NA KUWALEA KWA KUFATA MISINGI YA KITABU KITUKUFU CHA QUR-AN ILI KUPATA VIONGOZI WALIOBORA WA BAADAE
Alhajj Hemed ameyasema hayo alipokuwa akiwasalimia Waumini wa Masjid IMANI uliopo MIGOMBANI CHINI mara baada ya kumaliza Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Amesema kuwa wazazi na walezi wana jukumu kubwa la kuwasimamia vijana wao pamoja na kuwapatia elimu zote mbili ya dunia na akhera kwa manufaa yao wenyewe na Taifa kwa ujumla jambo ambalo litapelekea kupata viongozi bora wa Serikali pamoja na wanazuoni wenye kuisimamia dini ya kiislamu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema ni lazima kwa kila mzazi na mlezi kuhakikisha anawasimamia vijana wake ili kuwakinga na matendo maovu na machafu yatakayosababisha uvunjifu wa amani sambamba na kuwakinga na matendo ya uzalilishaji na madawa ya kulevya.
Alhajj Hemed amesema kuwa dunia imekumbwa na mambo mabaya na maovu mengi ambayo husababisha kuwepo kwa mmong’onyoko wa maadili hivyo ni wajibu wa kila mzazi na mlezi kumpatia kijana wake elimu ili kumuwekea msingi nzuri wa kimaisha hapo baadae.
Sambamba na hayo Alhajj Hemed amewashukuru Watanzania wote pamoja na Wazanzibari kwa kuendelea kudumisha amani, upendo na mshikamano baina yao jambo ambalo linaipelekea Serikali kufikia malengo yake iliyojiwekea ya kuwaletea maendeleleo endelevu wananchi wake.
Amesema ni lazima wananchi kuunga mkono jitihada zinazochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Nane (8) inayoongozwa na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika kuwaletea maendeleo wananchi wake pamoja na kuwatatulia chongamoto mbali mbali zilizokuwa ziwakabili bila ya ubaguzi wa aina yoyote.
Mapema akitoa Khutba katika Sala ya Ijumaa, Maalim ABDI ZUBEIR amewataka waumini wa dini ya Kiislam na Wazanzibari kwa ujumla kuhakikisha wanawapatia watoto haki zao za msingi jambo ambalo litapelekea kupata watoto walio wema pamoja na viongozi wazuri wa baadae.
Amesema kuwa kila mzazi na mlezi ni dhamana kwa anaemuongoza na ndio masuuli mkubwa kesho mbele ya haki hivyo ni lazima kuhakikisha anamsimamia vyema mtoto wake pamoja na anaowaongoza ili kupata radhi za Allah (S.W).
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
29-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
29-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
29-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
29-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
29-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
29-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
29-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
29-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
29-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
29-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
29-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
29-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
29-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
29-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
29-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
29-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
29-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
29-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
29-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
29-05-2026