MHE. HEMED SULEIMAN ABDULLA AMEFANYA ZIARA YA USIKU KUKAGUA MIRADI YA UJENZI WA MASOKO MAGHARIBI “B”
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amefanya ziara ya Usiku kukagua Miradi ya Ujenzi wa masoko ya Mwanakwerekwe na Jumbi Wilaya ya Magharibi “B” kujionea maendeleo ya miradi hiyo.Mhe. Hemed amesema hatua iliyofikia katika ujenzi wa masoko hayo ni ya kuridhisha ambapo amewataka wakandarasi na washauri elekezi kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilika kwa wakati uliopangwa na ubora wa hali ya juu .Amesema mategemeo ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuwa masoko hayo yakamilike mwishoni mwa mwaka huu ili wafanyabiashara waweze kuyatumia kwa shughuli za kujipatia kipato cha kila siku.
Aidha amemshukuru Rais Dkt. Mwinyi kwa miongozo anayoitoa katika miradi hiyo pamoja na upatikanaji wa fedha kwa wakati bila ya ucheleweshaji hatua ambayo inawapa moyo wakandarasi kuwa na kasi ya ujenzi huo. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ameeleza kuwa lengo la kujenga masoko hayo ni kuwawekea mazingira mazuri wafanyabiashara na wananchi ili waweze kufanya biashara zao kwa usalama wa afya zao na kuepuka kufanyabiashara katika maeneo yasiyo rasmi.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewaagiza Wakurugenzi wa Manispaa kuhakikisha wanatoa elimu na maelekezo kwa wafanyabiashara juu ya namna bora watakavyoyatumia masoko hayo na kuacha kufanya biashara pembezoni mwa barabara kwani Serikali imetumia gharama kubwa kuyajenga masoko hayo hivyo umakini unahitajika katika kuyatumia na kuyatunza masoko hayo.
Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara maalum za SMZ Mhe. Massoud Ali Moh'd amesema ziara hiyo ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar inaongeza ari na hamasa ya kufanya kazi kwa ustadi wa hali ya juu ili kufiki malengo ya Serikali kuwawekea mazingira mazuri wafanyabiashara. Ameeleza kuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amekuwa akishahuri na kutoa miongozo inayochangia kuharakisha umalizikaji wa ujenzi wa mradi wa masoko hayo.Kwa upande wake msanifu majengo na mshauri elekezi kutoka Wakala wa Majengo Zanzibar Mhandisi Shadya Fauz Muhamed amemueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kuwa tayari wakandarasi wapo hatua za mwishoni za kumalizia ujenzi huo na tayari vizimba vimeshaanza kujengwa.
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
27-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
27-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
27-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
27-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
27-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
27-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
27-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
27-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
27-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
27-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
27-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
27-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
27-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
27-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
27-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
27-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
27-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
27-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
27-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
27-05-2026