DK.HUSSEIN ALI MWINYI AMEZINDUWA MRADI WA KUWAJENGEA UWEZO VIJANA ILI WAWEZE KUJIAJIRI NA KUAJIRIKA KATIKA SEKTA YA UCHUMI WA BULUU
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imeeleza dhamira yake ya kuleta mageuzi makubwa kwenye sekta ya elimu kupitia Wizara yake ya Elimu na Mafunzo ya Amali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi alieleza dhamira hiyo kwenye ufunguzi wa mradi wa kuwajengea uwezo vijana kwa lengo la kuwawezesha kujiajiri na kuajirika kwenye sekta ya uchumi wa buluu huko ukumbi wa Golden Tulip, Uwanja wa ndege, Zanzibar.
Dk. Mwinyi alisema, Serikali inaendeleza jitihada mbali mbali kwa kuhakikisha inatoa elimu bora nchini katika kufikia dhamira hiyo kwa kuchukua hatua za kuboresha miundombinu ya skuli mpya ikiwemo ujenzi wa Skuli mpya za ghorofa kwa Unguja na Pemba na mafunzo kwa walimu.
Hatua nyengine, Rais Dk. Mwinyi alieleza ni kuzipatia huduma muhimu skuli hizo ikiwemo, upatikanaji wa vifaa bora vya kufundishia na kujifunzia, matumizi bora ya TEHAMA na kuwapatia vijana ujuzi na maarifa utakao wawezesha kuyakabili maisha yao na kunyanyua uchumi wa nchi.
“Kama hatutowaandaa vijana wetu, wakawa weledi wa kujua wanachokifanya, hatutofikia dhamira yetu ya kuhakikisha watu wote wakiwemo vijana wanashiriki na kunufaika na Uchumi wa Buluu” aliasa Rais Dk. Mwinyi.
Dk. Mwinyi alitaja sehemu ya ujenzi wa mradi huo ni pamoja na ujenzi wa Chuo cha kisasa cha Ubaharia na majengo utawala, ujenzi wa hosteli ya wanafunzi wa kike kwenye Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Karume yenye ukubwa wa ghorofa tatu na uwezo wa kuhudumia wanafunzi 500 kwa wakati mmoja, ujenzi wa madarasa ya kusomea na karakana zinazohusiana na masomo ya mafuta na gesi.
Aliongeza ujenzi wa vyuo vya mafunzo ya amali na vifaa vyote vinavyohitajika kwa programu zitakazotolewa na vyuo hivyo ambavyo vinatarajiwa kujengwa kwenye Wilaya za Mkoani (Chambani), Wilaya ya Micheweni (Tumbe Mashariki), Wilaya ya Kati (Jendele) na Wilaya ya Kaskazini B (Panga Tupu).
Shughuli nyengine za mradi huo wa SEBEP, Rais Dk. Mwinyi alizitaja ni pamoja kuwajengea uwezo watendaji wa Taasisi zinzozoshiriki kwenye mradi huo kwa kuwapatia nafasi za kuongeza taaluma zao, ujenzi wa kituo cha kuwapa vijana mafunzo ya kuanzisha na kuendeleza biashara zao (incubation centre) na vifaa vyake eneo la Kizimbani Unguja, ambacho kitakuwa chini ya usimamizi wa Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (ZEEA) na taasisi ya SMIDA imepewa jukumu la kuwapatia mafunzo mbalimbali vijana hao.
Rais Dk. Mwinyi alisema hatua hiyo inatoa nafasi kwa Vijana wa Zanzibar kupata fursa ya mafunzo ya amali na ufundi wa fani mbali mbali zikiwemo zinazohusiana na Uchumi wa Buluu.
Pia alitoa wito kwa vijana kuitumia vyema fursa ya mradi huo kujipatia ujuzi ili wanufaike na soko la ajira kwenye sekta ya uchumi wa buluu kwa kuweza kujiari na kupata sifa za kuajiriwa.
Dk. Mwinyi alisema mradi huo utaongeza upatikanaji wa wafanyakazi wenye taaluma kwenye shughuli za Utalii ambayo ni Sekta kiongozi katika uchumi wa Zanzibar pamoja na kuiwezesha Zanzibar kuzitumia vyema rasilimali zake za asili ikiwemo bahari, mafuta na gesi asilia katika kukuza pato la taifa na upatikanaji wa ajira kupitia sekta ya Uchumi wa Buluu.
Mradi wa kuwajengea uwezo vijana kwa lengo la kuwawezesha kujiajiri na kuajirika kwenye sekta ya uchumi wa buluu SEBEP unafadhiliwa kwa asilimia 90 na washirika wa maendeleo (AfDB) na asilimia 10 unafadhiliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, unatarajiwa kutumia dola za Marekani milioni 54 sawa na fedha za Tanzania shilingi bilioni 126.379.
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
28-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
28-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
28-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
28-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
28-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
28-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
28-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
28-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
28-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
28-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
28-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
28-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
28-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
28-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
28-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
28-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
28-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
28-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
28-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
28-05-2026