Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewataka wakandarasi wanaopewa dhamana ya kujenga Miradi ya Maendeleo Zanzibar kuheshimu Mikataba ya makubaliano wanayokubaliana kati ya Serikali na Kampuni husika
Ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Ofisi Kuu ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) lililopo Maisara Wilaya ya Mjini Unguja ikiwa ni muendelezo wa ziara zake za kutembelea na kukagua Miradi ya Maendeleo.
Mhe. Hemed amesema kumekuwa na tabia iliyozoeleka kwa baadhi ya wakandarasi kuchelewesha kumaliza kwa wakati miradi wanayopewa kujenga na kuomba kuongezewa muda jambo ambalo linakwamisha adhma ya Serikali ya kutatua kero za wananchi kwa wakati.
Amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuheshimu mikataba inayoingia na makampuni mbali mbali pamoja na kutoa ushirikiano wa hali ya juu kwa kampuni zinazojenga miradi ya maendeleo nchini ili kuharakisha ukamilishaji wa miradi hio kwa utaratibu uliopangwa na viwango vyenye ubora.
Makamo wa Pili wa Rais amesema kumalizika kwa wakati kwa ujenzi wa jengo hilo kutatoa fursa kwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kufanya kazi zao katika mazingira mazuri na salama kulingana na umuhimu wa ofisi hio.
Sambambana hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuanzia sasa Wakala wa Majengo Zanzibar (ZBA) wanapaswa kuwachukulia hatua stahiki Kampuni ambayo haitokabidhi Miradi kwa wakati uliopangwa ili iwe fundisho kwa kampuni nyengine zinazoendelea na ujenzi wa miradi mbali mbali hapa Zanzibar.
Aidha amewataka wakala wa majengo kuacha muhali kwa kampuni yoyote itakayo kwenda kinyume na mkataba wa ujenzi wa miradi ya Serikali ambayo imefungwa baina ya serikali na kampuni husika.
Nae mkandarasi kutoka kampuni ya China Railway Jianhuwang Engineering (CRJE) Chey Yur amesema licha ya kukabiliwa na changamoto mbali mbali mwanzoni mwa ujenzi huo lakini watahakikisha wanakamilisha na kukabidhi Jengo hilo ndani ya muda waliokubaliana.
Mkandarasi Yur amesema wameshaongeza nguvu kazi katika ujenzi huo na wanatarajia kuanza kufanya kazi usiku na mchana ili kuongeza kasi ya ujenzi na kukamilisha kwa wakati uliopangwa na kwa ubora zaidi.
Kwa upande wake msimamizi wa Majengo kutoka (ZBA) Mohamed Nahoda Mohamed amesema ZBA wamekuwa wakishirikiana kwa karibu na Mkandarasi wa ujenzi huo ambao kwa sasa umefikia asilimia 20% ya ujenzi na wanatarajia kukamilisha mwishoni mwa mwezi Disemba mwaka huu.
Ujenzi huo wa Jengo la Ghorofa 4 la Ofisi Kuu ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar utakapokamilika utagharimu zaidi ya Bilioni 11 ambao utajumuisha Ofisi, Kumbi za Mikutano na Vyumba kwa ajili ya wageni
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
27-02-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
27-02-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
27-02-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
27-02-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
27-02-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
27-02-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
27-02-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
27-02-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
27-02-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
27-02-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
27-02-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
27-02-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
27-02-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
27-02-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
27-02-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
27-02-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
27-02-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
27-02-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
27-02-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
27-02-2026