SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar, imesema inakusudia kuifanya Zanzibar kuwa kituo kikubwa cha Utalii wa kisasa usio na misimu kwa kuwavutia wawekezaji na wageni wengi.
Imesema Zanzibar bado inawakaribisha wawekezaji zaidi kwani ina maeneo mengi ambayo hayajafikiwa kwa kwa fursa nyingi za uwekezaji.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasea hayo Ikulu – Zanzibar alipozungumza na Balozi mpya wa Uingereza nchini Tanzania Mhe. Marianne Young alikuja kujitambulisha.
Dk. Mwinyi amesema bado ina Zanzibar ina uhitaji mkubwa wa uwekezaji kwenye sekta ya Uchumi wa Buluu kupitia Utalii, Bandari, Mafuta na gesi pamoja na sekta ya usafirishaji wa majini.
Ameeleza kwa muda mrefu Zanzibar imekua ikitangaza Utalii wa zamani wa Urithi ukiwemo wa Mji Mkongwe wa Zanzibar na Fukwe, ameongeza kuwa wakati umefika Zanzibar sasa kuendelea kujitangaza pia na utalii wa kisasa ukiwemo utalii wa mikutano ya kimataifa, michezo, akitolea mfano michezo ya mbio za magari ambao umekua kivutio kikubwa duniani na kuwavutia mashabiki na wageni wengi maarufu kama (Formula one).
Aidha, Rais Dk. Mwinyi amesema dhamira ya Serikali ni kuwa na Utalii wa hadhi ya juu utakaowavutia wageni wengi kuja nchini bila kujali misimu ya utalii, pia amesema nchi imejiandaa kuwa na misimu yote ya Utalii kwa kuimarisha vivutio zaidi vyenye kuwavutia wageni wengi.
Kuhusu ongezeko la Utalii Dk. Mwinyi ameeleza dhamira ya Serikali kuendelea kuimarisha miundombinu ya barabara na mawasiliano ikiwemo viwanja vya ndege vya Unguja na Pemba kuemdelea kuwa na hadi ya kimataifa.
Akizungumzia masuala ya Uchumi na Uwekezaji Rais Dk. Mwinyi amesema Bado kuna maeneo mengi ya Uchumi ambayo wawekezaji wakija wanaweza kushirikiana na Serikali kuyaendeleza.
Kuhusu Bandari, Dk. Mwinyi amezizungumzia fursa za Bandari jumuishi kwa Zanzibar ambayo Serikali imewekeza nguvu kubwa huko Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja alikoeleza kwa sasa Zanzibar inahitaji Bandari kubwa ili kukidhi mahitaji ya uchumi wake kama kituo muhimu cha usafirishaji, usambazaji wa bidhaa, kutoa huduma na kufanyia biashara ikiwemo kupokelea mizigo, kusafirishia mazao, na mahitaji mbalimbali ikiwemo mafuta, nafaka, na kukuza uchumi wake.
Kwa upande mwengine Rais Dk. Mwinyi aligusia suala la mafuta na gesi pamoja na sekta ya usafirishaji wa majini, akieleza Zanzibar inavyohitaji uwekezaji mkubwa kwenye sekta hiyo na kuiomba Serikali ya Uengereza kuangalia uwezekano wa kuungamkono kwenye sekta hiyo kuimarisha sekta ya biashara na uchumi wa Zanzibar kupitia bandari zake za Uguja na Pemba.
Dk. Mwinyi pia aligusia eneo la nishati na kumueleza mgeni wake huyo kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inadhamiria kuwa na umeme wa ukahkika kwa kuwa na umeme mbadala kwa ajili ya wawekezaji waliopo, hivyo, ameiomba Serikali ya Uingereza kuangaliua uwezekano wa kuweka nguvu zake kwenye eneo hilo.
Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi amewakaribisha wawekezaji zaidi wa Uingereza kuja Zanzibar kwa wingi kuwekeza na kunufaika na fursa za uwekezaji zilizopo.
Akizungumzia ukulima wa mwani, Dk. Mwinyi amemueleza balozi huyo kwamba Zanzibar inauza zao hilo kama malighafi kiasi ya kuwa halileti tija kwa Uchumi wa taifa na wakulima kwa ujumla, hivyo aliwashawishi wawekezaji kutoka Uingereza waje nchini waanzishe viwanda vya kuusarifu mwani na kuzalisha bidhaa za zao hilo jambo ambalo litawaongezea tija wakulima wa zao hilo nchini na bidhaa wanazozizalisha.
Pia amewaalika wawekazaji wa sekta binafsi wa Uingereza kuitembelea Zanzibar kubaini uzuri na fursa zilizopo.
Wakati huo huo, Rais Dk. Mwinyi ameishukuru Serikali ya Uingereza kwa ushirikiano wa diplomasia uliopo baina yao na Tanzania ikiwemo Zanzibar pia kwa kuisaidia Zanzibar kwa sekta mbalimbali ikiwemo Elimu, Afya na masuala mengine ya jamii.
Naye Balozi Marianne Young amemuhakikishia Rais Dk. Mwinyi kuwa Serikali ya Uingereza itaendelea kuunga mkono Zanzibar kuimarisha ustawi wa kuleta maendeleo hasa kwa masuala ya afya, elimu na Uchumi wa Buluu.
Amesema, Utalii ni fursa muhimu baina Zanzibar na Uingereza katika kuimarisha ushirikiano wa pande mbili hizo na kuiahidi Zanzibar kushirikiana kiufundi kwa uzoefu kwa masuala mbalimbali ya Uchumi, jamii na teknolojia.
Pia Balozi Young alisifu juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa maendeleo makubwa iliyofikiwa hasa kwa sekta ya mawasilino na miundombinu.
Alieleza Imani yake ya kuendeleza ushirikiano uliopo baina yao na kuahidi uuendeleza kwa vitendo na utekelezaji katika kuyafikia malengo baina ya pandembili hizo.
Balozi Marianne Young amechaguliwa wadhifa huo kuhudumu Tanzania mwezi Ogasti mwaka huu.
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
27-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
27-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
27-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
27-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
27-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
27-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
27-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
27-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
27-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
27-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
27-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
27-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
27-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
27-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
27-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
27-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
27-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
27-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
27-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
27-05-2026