RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Al hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewahimiza viongozi na watumishi wa umma kubadilika kwa kujikurubisha mbele ya Mwenyezi Mungu (S.W) ili kupata radhi zake katika kulitumikia taifa kwa haki na uadilifu.
Al hajj Dk. Mwinyi, ametoa nasaha hizo aliposhiriki kwenye Kongamano la kiimani kwa viongozi na watendaji wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar lililofanyika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul Wakil, Kikwajuni Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi.
Aidha, Al hajj Dk. Mwinyi alieleza, maratajio yake baada ya kongamano hilo ni kuona mabadiliko makubwa ya kiutendaji kwa watumishi na wateule aliowapa majukumu ya kumsaidi kwenye utendaji na weledi wa kufanyakazi za kuwatumikia watu. “Ni matarajio yangu tutatoka na kitu tofauti hapa mara baada ya kongamano hili kwani limemgusa kila mmoja wetu, kazi iliopo mbele ni muhimu kujitathmini na kurekebisha mapungufu yaliopo.” alisihi Al hajj Dk. Mwinyi.
Akizungumza masuala ya utawala bora, nidhamu na maadili kwenye utumishi wa umma alieleza, ni msingi imara wa kutengeneza badala ya kulete maafa kwa kukosekana vyote hivyo. Dk. Mwinyi alilaumu ukiukwaji wa nidhamu ya utumishi wa umma unaofanywa na baadhi ya viongozi pamoja na kusifu nidhamu iliyopo kwa baadhi ya vyombo vya ulinzi na usalama, hivyo aliwasihi viongozi na watumishi wa Serikali kujenga uaminifu, maadili na kutenda haki kwa hofu ya kumuogopa Mwenyezi Mungu.
Akizungumzia masuala ya usimamizi wa Kodi, Al hajj Dk. Mwinyi alisisitiza haja ya kuzisimamia kwa haki na uadilifu wa hali ya juu sio kudhulumu watu. Alisema, kodi ni muhimu kwenye kufanikisha huduma bora za jamii na kueleza umuhimu wake umetajwa kwa kina kwenye hata kwenye vitabu vitukufu vya dini.
Naye, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman alisifu kongamano hilo kuwa ni darasa lililowafunza viongozi wengi na kuwakumbusha kwenye wajibu wao wanaopaswa kutumikia umma kwa uadilifu kila
siku. Akizungumza kwenye Kongamano hilo, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi, Mhandis Zena Ahmedi Saidi aliwataka watumishi wa umma kuwa Sehemu ya mabadiliko makubwa ya utendaji Serikali na kuwatumikia watu.
Mhandisi Zena pia aligusia suala la uadilifu na kueleza kuwa halipo kwenye vipimo vya bidhaa pekee hata kwenye utedaji na utumishi wa Umma akiwazungumzia watumishi wanaochakata masaa ya utumishi kwa kutoyakamiisha kwa uadilifu ni ukosefu wa
uadilifu na upungufu wa imani ya dhati mbele ya Mola (S.W). Hivyo, aliwaeleza viongozi za Serikali na watumishi wa umma kujitafakari na kujitathmini wanapovunja uaminifu kwenye utendaji wao sambamba na kuwaeleza kuwa wanabeba dhima kubwa kwa Mwenyezi Mungu kwa kutokuwa waadilifu kwenye kazi zao.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye kongamano hilo lililokuwa na mnasaba na imaani za dini, Masheikh tofauti kutoka Tanzania na Mombasa, Kenya wakiwemo Sheikh Muhamad Al Hajir na Sheikh Izudin Alwy kutoka Kenya, Sheikh Nurdin Kishki
wa Dar es Salaam, Sheikh Shaaban Batash kutoka kamati ya Baraza la Maulamaa na Sheikh Khamis kutoka Kitengo cha Fatwa Ofisi ya Mufti, Zanzibar, waligusia masuala mbalimbali ya utumishi Serikalini ikiwemo nidhamu, ubinaadam kwenye uongozi,
utendaji, dhamana za vyeo, rushwa, uwajibikaji, uadilifu, kutunza siri na rasilimali za umma kwa mujibu wa nyadhifa wanazozitumikia, upendo, umoja, mshikamano na ushirikiano, kujiepusha na hasadi na tamaa ni msingi ya uongozi bora kwenye utumishi
wa umma.
Kongamano hilo la kiimani kwa viongozi na watendaji wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar lilitayarishwa na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar na kuratibiwa na Ofisi ya Mufti, Zanzibar lilikudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar.
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
28-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
28-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
28-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
28-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
28-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
28-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
28-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
28-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
28-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
28-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
28-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
28-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
28-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
28-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
28-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
28-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
28-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
28-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
28-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
28-05-2026