Wazazi na walezi wametakiwa kuwalea watoto wao katika maadili mema ili kupata kizazi chenye hofu ya Allah kitakachosaidia kuziondosha changamoto zilizopo zinazosababishwa na kukosekana kwa maadili mema kwa vijana.
Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla wakati akiwasalimia waumini wa Masjid JAMII WATHABATUL- KHEIR iliyopo KOANI kwa KOZI Wilaya ya Kati mara baada ya kumaliza Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Amesema ni wajibu wa kila mzazi na mlezi kuwalea watoto wao katika maadili mema yatakayowajenga kidini na kiimani jambo ambalo litasaidia Taifa kupata viongozi bora wa baadae na wenye kufanya kazi zao kwa hofu ya Mwenyezi Mungu.
Alhajj Hemed amesema wakati umefika wa jamii kujitathmini katika malezi wanayowalea watoto wao ili kupunguza malalamiko ya mmong’onyoko wa maadili unaopelekea vijana kujiingiza katika vitendo viovu ikiwemo udhalilishaji na utumiaji wa madawa ya kulevya.
Sambamba na hayo Alhajj Hemed ameendelea kuwasisitiza wananchi wa Zanzibar na Watanzania kwa ujumla kuzidi kudumisha Amani na Utulivu uliopo nchini jambo ambalo huwaweka huru katika kufanya shuhuli zao mbali mbali za kujitafutia maisha kwa faida yao na Taifa kwa ujumla.
Mapema akitoa Khutba katika Sala ya Ijumaa, Sheikh SALIM MASSOUD SEIF amewataka waumini wa Dini ya Kiislam kuendelea kuzilea vyema familia zao ili kuweza kupata watoto wema ambao watakuwa wema sasa na hadi kuondoka kwao duniani.
Amesema kuwa waislamu ni lazima kushirikiana na kuamrishana mambo mema na kukatazana mabaya ili kujikurubisha karibu na Allah (S.W) na kufikia lengo la kuumbwa mwandamu hapa duniani
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
28-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
28-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
28-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
28-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
28-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
28-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
28-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
28-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
28-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
28-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
28-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
28-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
28-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
28-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
28-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
28-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
28-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
28-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
28-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
28-05-2026