MIAKA MITATU YA DK.MWINYI YAANDIKA HISTORIA MPYA YA ZANZIBAR AMESEMA MBETO
KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, amesema kuwa miaka mitatu ya Uongozi wa Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi,inaiweka Zanzibar katika orodha ya nchi za visiwa zinazoendelea kwa kasi kubwa kiuchumi.
Hayo ameyasema wakati akizindua bonanza la kupongeza miaka mitatu ya uongozi wa Rais Dk.Mwinyi,lililoandaliwa na Mwakilishi wa Jimbo la Chwaka Mhe.Ussi Haji Gavu kwa kushirikiana na UVCCM Wilaya ya Kati Unguja, katika Chwaka.
Mbeto, alisema maendeleo yaliyofikiwa hivi sasa nchini katika nyanja za kiuchumi,kisiasa na kijamii ni kielelezo cha kujivunia utawala bora unaofuata sheria,utu na haki za binadamu unaosimamiwa na Serikali ya awamu ya nane chini ya Uongozi wa Dk.Mwinyi.
Alifafanua kwamba mafanikio hayo katika sekta za elimu,afya,kilimo,maji safi na salama,miundombinu ya usafiri wa anga,majini na nchi kavu sambamba na ujenzi wa barabara za kisasa mijini na vijijini vinatakiwa kulindwa na kuthamini ili viwe na manufaa kwa wananchi wote.
“Dhamira ya bonanza hili ni kupongeza miaka mitatu ya uongozi wa Rais wetu Dk.Hussein Mwinyi, amefanya mambo makubwa ya kimaendeleo hapa nchini kila mwananchi ananufaika kwa namna yake, tuendelee kumuunga mkono na kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumu.”alisema Mbeto.
Katika maelezo yake Katibu huyo wa NEC Zanzibar Mbeto, alisema ndani ya miaka mitatu ya uongozi wa Dk.Mwinyi, tayari Serikali imevuka malengo ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025.
Kupitia bonanza hilo aliwapongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Samia Suluhu Hassan, pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali, Mwinyi kwa kasi yao kubwa ya kiutendaji inayotoa muelekeo wa kupatikana kwa ushindi mkubwa wa Dola mwaka 2025.
Bonanza hilo limejumuisha mashindano ya mbio za Baiskeli pamoja na mbio za Ngalawa ambapo washindi wa mashindano hayo wamekabidhiwa zawadi mbalimbali.
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
29-12-2025
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
29-12-2025
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
29-12-2025
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
29-12-2025
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
29-12-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
29-12-2025
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
29-12-2025
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
29-12-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
29-12-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
29-12-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
29-12-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
29-12-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
29-12-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
29-12-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
29-12-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
29-12-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
29-12-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
29-12-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
29-12-2025
TAARIFA KWA UMMA
29-12-2025