MITANO TENA NI KWA DK. SAMIA TU, WENGINE SUBIRINI KUCHUJWA - WASIRA
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, ‘Mitano Tena’ ni kwa mgombea urais, Dk. Samia Suluhu Hassan na Mgombea Mwenza wake, Dk. Emmanuel Nchimbi, lakini wabunge na madiwani wasubiri kuchujwa kupitia vikao vya Chama.
Ameeleza hayo leo Juni 11, 2025 alipokuwa akizungumza katika kikao cha ndani kilichohusisha viongozi wa CCM Wilaya ya Nyasa, katika mji wa Mbamba Bay mkoani Ruvuma ambako anaendelea na ziara ya kuimarisha Chama.
“Niwaambie wana CCM wenzangu tunaposema mitano tena ni kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa nafasi ya urais na mgombea mwenza wake Dk. Emmanuel Nchimbi lakini kwa wabunge na madiwani wasubiri mchujo ndani ya Chama na mwaka huu tumeongeza idadi ya wapiga kura. Kwa mfano hapa Nyasa walikuwa wapigakura za maoni 900 lakini sasa wako 1,3000.”
Wasira alisema kupata wagombea safi ndani ya Chama wa udiwani na ubunge ni vema wakachaguliwa kwa utaratibu wa haki huku akisisitiza ‘mitano tena’ sio kwa watu wote ”Sio kila mtu ni mitano tena bali mitano tena ni kwa Rais Samia, wengine tunachujana.”
Akifafanua zaidi, Wasira alisema mabalozi wa CCM wana kazi ya kuchagua wagombea safi kupitia kura za maoni ambao watauzika mbele ya wananchi na sio wagombea ambao wanatokana na kununua kura.
“Heshima ya wajumbe ni anayesikiliza watu walionyuma yake, ni kupiga kura kwa mtu ambaye wananchi wanamtaka na katika majina matatu ambayo yatapendekezwa kupitia kura za maoni atapatikana mmoja ambaye atakuwa diwani au mbunge kwa miaka mitano.
“Kuna diwani amesema hapa kuwa wamefanya kazi nzuri na wanaomba ruhusa waendelee. Hakuna mtu anakataa ruksa lakini ruhusa haitolewi na mimi bali inatolewa na wananchi waliokupigia kura. Mimi nikimaliza (ziara) naondoka lakini wapigakura wanabaki na ndio watasema diwani amefanya kazi nzuri tunataka arudi na wale wapigakura wa kata yako watasema hivyo ndivyo.”
Katika ziara hiyo Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Tanzania Bara Stephen Wasira amekagua maendeeo ya Ujenzi wa bandari ya Mbambabay iliyoko wilayani Nyasa mkoani Ruvuma ambayo Serikali imepeleka fedha ili kuiboresha.
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
28-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
28-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
28-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
28-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
28-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
28-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
28-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
28-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
28-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
28-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
28-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
28-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
28-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
28-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
28-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
28-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
28-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
28-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
28-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
28-05-2026