MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndugu Mohamed Ali Kawaida, amewataka Vijana waliopewa dhamana za kiutendaji ndani Chama na Serikali kufanya kazi kwa bidii ili kwenda sambamba na kasi ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025.
Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na Viongozi,Watendaji na Wanachama wa UVCCM Mkoa wa Magharibi katika mwendelezo wa ziara yake ya kuimarisha uhai wa Jumuiya hiyo huko Afisi kwao Mwera Unguja.
Alisema kuwa Vijana,wanatakiwa kuwa mfano bora katika masuala mbalimbali ya kujenga Taifa kimaendeleo.
Alisema lengo la ziara hiyo ni kuimarisha uhai wa Chama na Jumuiya hiyo, kukagua Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya Mwaka 2020/2025 na kuhakikisha changamoto zinazowakabili Vijana zinafutiwa ufumbuzi wa kudumu.
" Vingozi wetu Wakuu ambao ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi wametuamini Vijana na kutupatia dhamana mbalimbali hivyo nasi tunatakiwa kuonyesha uwezo wetu kwa vitendo. ",alisema Mwenyekiti huyo Mohamed Kawaida.
Alisema Serikali Kwa Sasa imejielekeza katika kufanya Mapinduzi ya kimaendeleo, kwa kufungua milango ya uwekezaji hasa katika miradi mikubwa ya kimkakati pamoja na Viwanda vitakavyotoa ajira za kudumu kwa Vijana na Wananchi kwa ujumla.
Katika maelezo yake Mwenyekiti huyo Mohamed, alisema pamoja na juhudi hizo za kuleta maendeleo endelevu nchini bado Kuna makundi ya wanasiasa wasiokuwa wazalendo wanaendelea kubeza na kutoa kauli za kuwachonganisha Wananchi na Serikali zao.
Kupitia Kikao hicho Mohamed Kawaida, aliwapongeza Vijana wa Mkoa huo kwa kazi kubwa wanayofanya ya kuimarisha Jumuiya na Chama kwa ujumla.
Katika ziara hiyo Mwenyekiti huyo amefuatana na Viongozi wa Kamati tekelezaji ya UVCCM Taifa, Wabunge, Wawakilishi na Wajumbe wa NEC wanaotoka katika Umoja huo.
Mohamed Kawaida ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, katika Mkoa huo amekagua Hospitali ya Wilaya ya Magharib 'B', Kukagua Kituo cha Ujasiriamali na UVCCM, kushiriki ujenzi wa Tawi la CCM Tomondo Uzi, kushiriki ujenzi wa Tawi la CCM Bilikani na kuzindua kundi la hamasa la Vijana Fuoni.
Maeneo mengine ni kukagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Polisi Wadi ya Kipungani, maendeleo ya ujenzi wa Soko la Jumbi, kukagua Kituo cha Ujasiriamali Bweleo, kuweka jiwe la msingi katika Maskani ya Maungani, kuongea na Vijana wanaoendesha mradi wa kukusanya takataka pamo
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
27-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
27-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
27-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
27-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
27-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
27-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
27-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
27-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
27-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
27-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
27-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
27-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
27-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
27-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
27-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
27-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
27-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
27-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
27-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
27-05-2026