CHONGOLO AMSHITUKIA MKANDARASI KUSUASUA UJENZI WA BARABARA YA KIBAONI-STALIKE MLELE
*Ahoji mkandarasi kukwangua barabara aliposikia ujio wake
*Atoa maelekezo kwa DC ‘kushughulika’ na Mchina anayejenga
*Ang’aka akiwataka watendaji kusimamia fedha za umma kwa uchungu zilete matokeo
Mpimbwe, Mlele, Katavi
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Komredi Daniel Chongolo ‘amemshtukia’ Mkandarasi anayejenga Barabara ya Kibaoni - Stalike, kwa kiwango cha lami, baada ya kukagua na kushuhudia ujenzi wa barabara hiyo ukisuasua na kuwa nyuma ya muda, kinyume cha mkataba.
Kufuatia hali ya kusuasua kwa ujenzi wa barabara hiyo muhimu inayotarajiwa kuufungua zaidi Mkoa wa Katavi kuunganisha na mikoa mingine ya jirani na kuchochea zaidi shughuli za uchumi na uwekezaji wa wananchi wa maeneo hayo, ametoa maelekezo kwa Mkuu wa wilaya ya Mlele, Majid Mwanga, kukutana na uongozi wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mshauri Mwelekezi na Mkandarasi CSRG ili kuhakikisha kasi ya ujenzi inaongezeka kulingana na mkataba.
Chongolo ametoa maelekezo hayo baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo iliyopo wilayani Mlele, Katavi Oktoba 4, 2023, akiendelea na ziara yake ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020 - 2025 na kusikiliza changamoto za wananchi.
“Wakati wa kuhitimisha ziara yangu Oktoba 7, 2023, atakuja Waziri wa Ujenzi. Nimemuita tukutane Mpanda hapo, aje mwenyewe kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo na kuwaeleza wananchi ni namna gani barabara hiyo itakamilishwa kwa kasi inayotakiwa,” amesema Komredi Chongolo.
Barabara hiyo yenye urefu wa zaidi ya Km 50 itakayogharimu zaidi sh. Bil. 80, inajengwa na Kampuni ya China ya CRSG. Ujenzi wa barabara ulianza Juni 23, 2022 na unatarajiwa kukamilika Juni 22, 2025.
Akitoa taarifa kwa Katibu Mkuu wa CCM, kuhusu maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo, Kaimu Meneja wa TANROADS, Mkoa wa Katavi, Albert Laizer amesema kuwa hadi sasa umefikia asilimia 11.2 nyuma ya utekelezaji ambao ulipaswa uwe asilimia 21. Muda umefika miezi 15 kati ya 36 iliyopangwa. Na hadi sasa mkandarasi huyo ameshalipwa malipo ya awali zaidi ya sh. Bil. 12.
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
26-02-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
26-02-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
26-02-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
26-02-2026
πππ¦πππ‘ππ’ πππ πππ§. π ππππ₯π’ ππππ£π’πππππͺπ ππͺπ π¦πππ‘ππͺπ πππ₯ ππ¦ π¦πππππ
26-02-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
26-02-2026
π©ππππ‘π π§π¨ππππ‘ππ ππ ππ‘π π¬π π‘πππ π¬ππ§π¨ - π πͺππ‘πππ πππ‘ππ‘π
26-02-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
26-02-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
26-02-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
26-02-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
26-02-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
26-02-2026
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
26-02-2026
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
26-02-2026
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
26-02-2026
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
26-02-2026
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
26-02-2026
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
26-02-2026
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
26-02-2026
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
26-02-2026