CHONGOLO AMSHITUKIA MKANDARASI KUSUASUA UJENZI WA BARABARA YA KIBAONI-STALIKE MLELE
*Ahoji mkandarasi kukwangua barabara aliposikia ujio wake
*Atoa maelekezo kwa DC ‘kushughulika’ na Mchina anayejenga
*Ang’aka akiwataka watendaji kusimamia fedha za umma kwa uchungu zilete matokeo
Mpimbwe, Mlele, Katavi
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Komredi Daniel Chongolo ‘amemshtukia’ Mkandarasi anayejenga Barabara ya Kibaoni - Stalike, kwa kiwango cha lami, baada ya kukagua na kushuhudia ujenzi wa barabara hiyo ukisuasua na kuwa nyuma ya muda, kinyume cha mkataba.
Kufuatia hali ya kusuasua kwa ujenzi wa barabara hiyo muhimu inayotarajiwa kuufungua zaidi Mkoa wa Katavi kuunganisha na mikoa mingine ya jirani na kuchochea zaidi shughuli za uchumi na uwekezaji wa wananchi wa maeneo hayo, ametoa maelekezo kwa Mkuu wa wilaya ya Mlele, Majid Mwanga, kukutana na uongozi wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mshauri Mwelekezi na Mkandarasi CSRG ili kuhakikisha kasi ya ujenzi inaongezeka kulingana na mkataba.
Chongolo ametoa maelekezo hayo baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo iliyopo wilayani Mlele, Katavi Oktoba 4, 2023, akiendelea na ziara yake ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020 - 2025 na kusikiliza changamoto za wananchi.
“Wakati wa kuhitimisha ziara yangu Oktoba 7, 2023, atakuja Waziri wa Ujenzi. Nimemuita tukutane Mpanda hapo, aje mwenyewe kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo na kuwaeleza wananchi ni namna gani barabara hiyo itakamilishwa kwa kasi inayotakiwa,” amesema Komredi Chongolo.
Barabara hiyo yenye urefu wa zaidi ya Km 50 itakayogharimu zaidi sh. Bil. 80, inajengwa na Kampuni ya China ya CRSG. Ujenzi wa barabara ulianza Juni 23, 2022 na unatarajiwa kukamilika Juni 22, 2025.
Akitoa taarifa kwa Katibu Mkuu wa CCM, kuhusu maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo, Kaimu Meneja wa TANROADS, Mkoa wa Katavi, Albert Laizer amesema kuwa hadi sasa umefikia asilimia 11.2 nyuma ya utekelezaji ambao ulipaswa uwe asilimia 21. Muda umefika miezi 15 kati ya 36 iliyopangwa. Na hadi sasa mkandarasi huyo ameshalipwa malipo ya awali zaidi ya sh. Bil. 12.
CCM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA
28-05-2026
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
28-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
28-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
28-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
28-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
28-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
28-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
28-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
28-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
28-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
28-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
28-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
28-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
28-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
28-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
28-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
28-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
28-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
28-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
28-05-2026