Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Hemed Suleiman amesema Serikali haijaridhishwa na kasi ya Ujenzi unaoendelea wa Skuli ya Sekondari ya Makunduchi jambo ambalo linarejesha nyuma dhamira ya Dkt. Hussein Mwinyi ya kuondoa changamoto zote za Elimu kwa wanafuzi wa Mikoa yote ya Zanzibar.
Ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa skuli ya Sekondari ya Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake ya kuitembelea skuli hio kila ifikipo mwisho wa mwezi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Serikali imeshailipa Kampuni ya Fuchs Contraction Limited shiling Bilioni 4.08 ili kuharakisha umalizikaji wa Ujenzi wa Skuli hiyo lakini kasi ya ujenzi bado inasuasua na kupelekea wanafunzi kuendelea kufuata huduma ya elimu maeneo ya mbali na makaazi yao.
Amesema kuwa endapo Mkandarasi kutoka kampuni ya Fuchs atashindwa kumaliza ujenzi wa skuli hio na nyenginezo amabazo zinajengwa na kampuni hio kwa wakati ambao wamekubaliana katika mkataba wao itakuwa wamejinyima fursa ya kufanya kazi ndani ya Zanzibar hasa katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Nane(8) na serikali haitalifumbia macho jambo hili.
Amesema lengo la Serikali ya Awamu ya Nane(8) inayoongozwa na Rais Dkt Hussen Ali Mwinyi ni kuondoa changamoto mbali mbali zinazowakabili wananchi ikiwa ni pamoja na kuwekeza zaidi katika Sekta ya elimu ambayo ndio muhimili mkuu wa maendeleo nchini.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amefika katika skuli ya Sekondari ya Hasnuu Makame kukagua maendeleo ya ukarabati wa jengo la dahalia ya wanawake liloungua moto na kusababisha hasara kubwa kwa wanfunzi wanaosoma skulini hapo, na kuwataka walimu na wanafunzi kuendelea kulitunza na kudumisha usafi ndani na nje ya jengo hilo ili liweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu kwa maslahi ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Mhe. Hemed ameuagiza Uongozi wa Wizara ya Elimu kuhakikisha ndani ya muda mfupi ujao wanaijengea uzio skuli hio ili kuimarisha ulinzi na usalama kwa wanafunzi wanaishi hapo sambamba na kumtaka Mkandarasi kutoka Kampuni ya Faster kuhakikisha anamalizia matengenezo madogo madogo yaliyobakia ndani ya siku tano(5) ili wanafunzi waweze kuhamia na kuendelea na masomo yao katika hali ya utulivu.
Nae Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Ali Abdulghulam Hussein amesema wizara imejipanga kuhakikisha inaipatia kila skuli vifaa vya kusomea vya kisasa ili kuboresha mfumo wa elimu Visiwani ZanzibarambapoWizara imefanya ununuzi wa vifaa mbali mbali ikiwemo vitanda zaidi ya elfu moja(1000) kwa ajili ya skuli ambazo zinamadahalia Kompyuta, Projecta, viti na meza ambavyo vyote vitagawiwa kwa skuli zote za Unguja na Pemba.
Mhe. Gulam ameiomba Serikali kuichukulia hatua ya kuipiga penalt Kampuni ya Fuchs kwa kusababisha kuchelewa kumalizika kwa Ujenzi wa Skuli nane (8) zinazojengwa na kampuni hio jambo ambalo litatoa fundisho kwa kampuni nyengine zitakazopatiwa fursa ya kufanya kazi na Serikali ya Awamu ya Nane (8).
Kwa upande wake Mkandarasi kutoka kampuni ya Fuchs Contraction Ltd Devid Mwasomola amesema changamoto kubwa iliosababisha kishindwa kuendelea na Ujenzi wa Skuli hio ni kukosekana kwa nondo na malipo kwa ajii ya wafanyakazi hivyo ameaahidi kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha kazi hio ndani ya muda uliopangwa kwa sasa.
Katika ziara hio Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametembelea ujezi wa skuli ya ghorofa (G+3) ya Sekondari ya Makunduchi inayojengwa na Kampuni Fuchs Contraction Limited, na kukagua maendeleo ya ukarabati wa jengo la dahalia ya wanawake katika Skuli ya Sekondari ya Hasnuu Makame liloungua moto na kusababisha athari kubwa kwa wanafunzi wanaoishi hapo mwishoni mwa mwaka jana.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
25-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
25-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
25-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
25-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
25-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
25-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
25-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
25-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
25-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
25-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
25-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
25-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
25-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
25-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
25-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
25-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
25-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
25-05-2026