Watanzania na waumini wa Dini ya Kiislamu kuhimizana kila wakati juu ya kuitunza amani iliopo nchini kwa faida ya vizazi vya sasa na baadae.
Ameyasema hayo alipokuwa akisalimiana na waumini wa Dini ya kiislamu katika Masjid KAHFI uliopo MKELE KWA BIMTORO Wilaya ya Mjini mara baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Alhajj Hemed amesema ili Taifa lipige hatua kimaendeleo ni lazima kuwepo na Amani na Utulivu ndani ya nchi, hivyo ni wajibu wa kila mwananchi wa Tanzania na muumini wa Dini ya kiislamu na dini nyengine kuhakikisha anaienzi na kuilinda Amani iliyopo nchini kwa faida ya vizazi vya sasa na baade pamoja na Taifa kwa ujumla.
Makamu wa pili amesema zipo nchi duniani hawawezi kujumuika pamoja katika kufanya ibada kutokana na kutokuwepo kwa amani na utulivu ndani ya nchi zao hivyo ni wajibu wa kila mwananchi kuhakikisha anaitunza tunu ya amani iliyopo kwa maslahi mapana ya Taifa letu.
Amesema ni lazima kujifunza kutoka kwa nchi za jiarani jinsi wanavyokosa amani kwa sasa jambo ambalo linapelekea kukosekana kwa maendeleo na kuwataka wananchi kutokubali kushawishiwa na baadhi ya watu wasioitakia mema nchi yetu hasa kipindi cha siasa.
Aidha Alhajj Hemed amewataka baadhi ya viongozi kuacha kutoa maneno ya uwongo na yauchochezi ambayo yanaweza kusababisha uvunjifu wa amani iliyopo nchini na kuwataka kuihubiri amani wakati wote ili kupata maendeleo kwa maslahi ya wananchi wote.
Sambamba na hayo Alhajj Hemed ameendelea kuwakumbusha waumini wa Dini ya Kiislamu na wananchi kwa ujumla kuendelea kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum wakiwemo mayatima, wajane na wazee wasiojiweza ili kuzidisha upendo baina yao.
Amesema ipo haja ya kuitumia misikiti kwa kuyatambua makundi haya muhimu ili kuweza kuyasaidia ikiwa ni njia moja wapo ya kudumisha upendo na ushirikiano na kuweka usawa wa kila mwannchi.
Mapema akitoa Khutba katika Sala ya Ijumaa, Maalim MUHITA ALI HASSAN amewataka waumini wa dini ya Kiislam kujitathmini na kujiangalia upya katika kufanya ibada hasa katika kipindi hichi cha kuukaribisha mwaka mpya wa kiislamu siku chache zijazo.
Amesema kuwa uislamu umewataka waumini kuhimizana katika kufanya ibada pamoja na kuwa wamoja kwa kila kitu hasa katika kuipigania dini ya kiislamu ili kuweza kufikia malengo ya kuletwa hapa duniani
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
26-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
26-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
26-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
26-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
26-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
26-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
26-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
26-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
26-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
26-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
26-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
26-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
26-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
26-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
26-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
26-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
26-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
26-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
26-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
26-05-2026