MJUMBE WA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA NDG. HEMED SULEIMAN ABDULLA AMEPONGEZA HATUA YA VIONGOZI WA JIMBO LA MWANAKWEREKWE KWA KUWASAIDIA VIJANA KUPATA UJUZI WA KUJIKIMU KIMAISHA
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndg. Hemed Suleiman Abdulla amepongeza hatua ya Viongozi wa Jimbo la Mwanakwerekwe kujenga kituo cha wajasiriamali ili kuwasaidia vijana kuweza kupata ujuzi na kujikimu kimaisha. Mhe. Hemed ameyasema hayo wakati alipotembelea kituo cha wajasiriamali Jimbo la Mwanakwerekwe ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kukagua uhai wa Chama katika Majimbo yote ya Uchaguzi ya Zanzibar. Amesema kuwepo kwa kituo hicho kunaunga mkono dhamira ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuwawekea mazingira mazuri wajasiriamali.
Ameeleza kuwa kituo hicho kinasaidia kuwapatia ujuzi vijana wa Jimbo hilo na majimbo mengine na hatimae kuzalisha ajira nyingi zitakazowanufaisha vijana wa Zanzibar. Akitoa taarifa ya Kituo cha Ujasiriamali Jimbo la Mwanakwerekwe Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu. Said Saleh Said ameeleza kuwa kituo hicho kimeanza rasmi mwaka 2022 kikiwa na lengo la kuwapatia elimu ya Ujasiriamali Vijana ili waweze kujiajiri pamoja na kujikimu kimaisha na kuondokana na mawazo potevu ya kujihusisha na Vikundi viovu.
Amesema tokea kuanzishwa kwake kituo hicho kimezalisha vijana wenye taaluma na uweledi mkubwa kwa kuzalisha bidhaa zilizo bora na zenye viwango pamoja na kuanzisha kitengo cha tehama kwa ajili ya kutoa elimu ya Habari na mawasiliano. Katika ziara hiyo Mjumbe huyo wa kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amezungumza na wanachama na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi na kueleza kuwa Jimbo la Mwanakwerekwe ni miongoni mwa Majimbo yaliyonufaika na miradi mingi ya kimaendeleo ambayo itawanufaisha wananchi wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote.
Aidha Mhe. Hemed amewasihi wazazi na walezi kuwasimamia vijana wao ambao wameshafikia umri wa kupata Vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi kuhakikisha wanpata itambulisho hivyo pamoja na kujitokeza kwa wingi wakati wa Daftari la kudumu la wapiga kura ili kukipatia ushindi Chama Cha Mapinduzi wakati wa uchaguzi. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Jimbo la Mwanakwerekwe Ramadhan Fatawi Issa amemshukuru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kuelekeza miradi mingi ya maendeleo katika Jimbo hilo ikiwemo Ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya Magharibi B, Skuli za Ghorofa, barabara za ndani, Soko la kisasa na ujenzi wa Barabara za juu (FLYOVER) zinazotarajiwa kujengwa mwanzon mwa mwezi huu.
Amesema ni dhahiri Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameamua kwa dhati kuwafikishia huduma bora wananchi wake.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
25-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
25-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
25-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
25-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
25-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
25-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
25-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
25-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
25-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
25-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
25-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
25-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
25-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
25-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
25-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
25-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
25-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
25-05-2026