NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amewataka viongozi wa chama na jumuiya wanaohusika na masuala ya uenezi,itikadi na mafunzo kwenda na wakati wa mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanayoleta tija katika ushindani wa kisiasa nchini
Wito huo ameutoa wakati akifungua mafunzo kwa makatibu wa siasa,uenezi,itikadi,hamasa na chipukizi pamoja na elimu na malezi wa Chama Cha Mapinduzi na jumuiya zake ngazi za majimbo,wilaya na mikoa minne ya CCM Unguja yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Fuji Bububu Zanzibar.
Dkt.Dimwa, ameeleza kuwa viongozi hao wana jukumu kubwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi kwani wanatakiwa kufafanua sera na miongozo,kuhamasisha,kueneza uetekelezaji wa ilani,kutoa mafunzo kwa wanachama pamoja na kujibu hoja mbalimbali za upotoshaji zinazotolewa na vyama vya upinzani kwa dhamira ya kuchafua na kuhujumu mambo mema yanayotekelezwa na Chama za serikali zake.
Alisema siasa za zama za sasa zinafanyika sana katika mitandao ya kijamii na zinasambaa kwa kasi kubwa kuliko katika majukwaa ya kisiasa ya kawaida na kwamba ni lazima viongozi hao waende sambamba na kasi hiyo katika kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi kuamini kuwa CCM ndio chama pekee chenye dhamira ya dhati ya kuwaletea maendeleo endelevu.
Katika maelezo yake amewasisitiza viongozi hao kuendeleza utamaduni wa kujibu hoja za wapinzani na kufafanua kwa undani utekelezaji wa ilani katika maeneo yao panapotokea jambo lolote la upotoshaji hasa kwa ngazi za majimbo,wilaya na mikoa na kuacha tabia za kusubiri kazi hizo zifanywe na ngazi za kitaifa pekee.
“Nasaha zangu kwenu fanyeni kazi kwa mujibu wa majukumu yenu jibuni hoja kwa hoja sio matusi wala ubabaishaji kwani chama chetu kinatekeleza majukumu yake kwa uhalisia zaidi kwa kila nyanja.
Tangazeni utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 namna ilivyofanyika katika maeneo yenu ili wananchi na wanachama wa chama cha mapinduzi, ambao ndio mtaji wetu wa kisiasa waelewe ili waweze kufanya maamuzi ya kuwapigia kura za ndio wagombea wetu katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2025”.alisema Dkt.Dimwa.
Kupitia hafla hiyo Dkt.Dimwa, alisisitiza viongozi hao kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uandikishaji wa daftari la wapiga kura kwa awamu ya pili ili kupata watu wenye sifa za kuwapigia kura wagombea wa CCM.
Aliwataka viongozi hao kuepuka makundi yasiofaa ya kutumiwa kwa maslahi binafsi na baadhi ya viongozi na wanachama ndani kwa dhamira ya kutengeneza migogoro isiyofaa ndani ya taasisi hiyo.
Pamoja na hayo alibainisha kuwa Chama Cha Mapinduzi kinahitaji wabunge,wawakilishi na madiwani imara wanaofanya kazi kwa ufanisi ya kuwahudumia na kwamba kiongozi yeyote asiyetekeleza majukumu yake chama hakitompa nafasi ya kuongozakatika uchaguzi mkuu ujao.
Alifafanua kuwa ibara ya 246 (e) katika Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 inaeleza umuhimu wa mafunzo ya makada na viongozi wa chama kwa kudumisha na kuandaa mafunzo ili kuendeleza na kukuza elimu ya itikadi na uzalendo kwa viongozi wa CCM.
Alisema CCM inaendelea na maandalizi ya kutekeleza ibara 5 ya katiba ya CCM ya mwaka 1977 toleo la mwaka 2022 inayoelekeza kuwa ushindi wa CCM ni lazima kwa ngazi zote katika uchaguzi wa serikali za mitaa pamoja pamoja na uchaguzi mkuu wa wa dola.
Naye Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya itikadi,uenezi na mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwaandaa na kuwajengea uwezo makatibu hao wakafanye kazi zao kwa ufanisi ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya upatikanaji wa ushindi mwaka 2025.
“Tunaposema hakuna mbadala wa Dk.Mwinyi 20125 tunaimanisha na sasa tunatesti mitambo yetu kwa kuandaa kimafunzo jeshi letu la kisiasa kwani mwaka mwezi octoba mwaka 2025 tunaingia katika vita ya kidemokrasia ambayo kwa tathimini zetu mpaka sasa kupitia kazi kubwa ya utekelezaji wa Ilani iliyofanywa na Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi tuna uhakika wa kupata ushindi wa zaidi ya asilimia 90”.alifafanua Mbeto.
Aliwashauri viongozi wa baadhi ya vyama vya upinzani nchini kuacha chokochoko zinazoashiria kuingiza Zanzibar katika machafuko badala yake nao watumie ruzuku wanazopata serikali kufanya maendeleo kuwepo kwa ushindaji wa kisera na kwamba maneno ya majukwaani hayana tija kwa wananchi.
Kuptia mafunzo hayo ziliwasilishwa mada nne zikiwemo mahusiano na vyombo vya habari,umuhimu wa matumuzi ya mitandao ya kijamii,wajibu na maadili ya viongozi wa Chama na Jumuiya(Maandalizi ya Daftari la kudumu la wapiga kura) na maandalizi ya Mikutano.
🔰VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA VYAIMARISHA MSHIKAMANO, DKT. DIMWA AHITIMISHA MAFUNZO MAALUM
25-05-2026
KATIBU WA NEC, ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO CCM TAIFA NDUGU KENANI KIHONGOSI AMNADI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI EMMANUELA KAGANDA MTATIFIKOLO
25-05-2026
MUENDELEZO WA MAFUNZO YA VIONGOZI KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE – KIBAHA
25-05-2026
SIKU YA KWANZA YA MAFUNZO KATIKA SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL.
25-05-2026
UFUNGUZI WA MAFUNZO YA VYAMA SITA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
25-05-2026
MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CPC, KOMREDI LIU HAIXING IKULU DAR ES SALAAM
25-05-2026
KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM
25-05-2026
CCM NA FRELIMO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI
25-05-2026
UZINDUZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA
25-05-2026
CCM YAIPA POLE MSUMBIJI KWA KUKUMBWA NA MAFURIKO
25-05-2026
INJINI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IPO MASHINANI; DKT.MIGIRO
25-05-2026
DK.MIGIRO:CCM INAJENGWA KUANZIA NGAZI YA MASHINA SIO MAJUKWAANI.
25-05-2026
𝗞𝗜𝗦𝗛𝗜𝗡𝗗𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗖𝗛𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗔𝗡𝗚𝗪𝗘 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠
25-05-2026
NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA AMWAKILISHA KATIBU MKUU WA CCM KWENYE MSIBA WA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO
25-05-2026
𝗩𝗜𝗝𝗔𝗡𝗔 𝗧𝗨𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗘 𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗬𝗘𝗧𝗨 - 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗘𝗭𝗜 𝗞𝗘𝗡𝗔𝗡𝗜
25-05-2026
DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WATEULE- IKULU CHAMWINO DODOMA
25-05-2026
WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA (GENERAL)
25-05-2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ..
25-05-2026
RAIS SAMIA AKIHUTUBIA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
25-05-2026