Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameutaka Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi (WCF) na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) kuendeleza ushirikiano katika kazi utakaoleta manufaa makubwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku
Akifungua kikao kazi kati ya Mahakama ya Tanzania, Mfuko wa hifadhi ya Jamii Zanzibar na Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Zanzibar Beach Resort, Mhe. Hemed amesema Taasisi hizo zinapaswa kuwa na maazimio ya pamoja katika kuzifanya maboresho mbali mbali sheria zote zinazohusiana na malipo ya fidia kwa wafanyakazi na taratibu zote zinazotumika katika kutoa huduma hio.
Mhe. Hemed amesema waajiri wote Tanzania Bara na Zanzibar wanapaswa kubeba dhamana kwa wafanyakazi wao pindi wanapopata majanga yatokanayo na kazi kwa kuchukua hatua za haraka ikiwemo kutoa taarikwa kwa WCF na ZSSF ndani ya muda uliowekwa kisheria ili wafanyakazi au wategemezi wao waweze kupata mafao stahiki kwa wakati.
Aidha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema uwepo wa Majaji wa Mahkama Kuu kwa pande zote mbili za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika kikao kazi hicho kinatoa fursa kwao kujifunza namna ya kufanya kazi na WCF pamoja na ZSSF hasa katika kuboresha huduma za kimahakama kwa kutambua hatua mbali mbali katika uchakataji wa madai ya wafanyakazi waliopata madhila yatokanayo na kazi wanzozifanya.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewahakikishia washiriki wa kikao kazi hicho kuwa Serikali zote mbili zitaendelea kutoa ushirikiano utakaohitajika katika kuboresha mahusiano yenye lengo la kuleta ustawi wa wafanyakazi pindi wanapokuwa kazini.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Vijana na watu wenye ulemavu MERY MAGANGA amesema vikao kazi kama hivi vinaumuhimu mkubwa sana katika kudumisha Muungano wa Tanzania pamoja na kuimarisha utendaji kazi kwa wafaanyakazi jambo ambalo huleta tija kubwa kwa Taifa.
MAGANGA amesema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu itaendelea kufanya kazi kwa ushirikiano kati ya pande zote mbili za Muungano kwa kuhakikisha sheria ya fao la Fidia linatekelezwa kwa haki na usawa kwa wafanyakazi wote sambamba na kuwataka washiriki wote wa kikao hicho kwenda kuyafanyia kazi kwa vitendo yale ambayo watakubaliana katika mkutano huo.
Nae Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Tanzania Mhe. MUSTAPHER SIYANI amesema lengo kuu la kikao kazi hicho kufanyika Zanzibar ni kudumisha Muungno na kuweka mazingira bora na rafiki yenye kuvutia wawekezaji hasa pakiwa na mfumo Imara wa utowaji na upatikaniji wa haki nchini.
SIYANI amesema kikao hiki kitawakumbusha Majaji, watendaji wa mahakama na wadau wa haki juu ya utekelezaji wa nguzo ya pili ya upatikanaji wa haki na kuwasaidia katika kutafuta utatuzi wa migogoro ya kazi katika Taasisi mbali mbali zilizopo nchini.
Mapema Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. JOHN MDUMA amesema Utiaji wa saini wa makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja kati ya WCF na ZSSF unathibitisha mahusiano imara waliyonayo kwa muda mrefu yanayodhihirisha utayari wa kuwasaidi wafanyakazi hasa pale wanapopata majanga wakiwa kazini.
Dkt. MDUMA amesema WCF wameona ipo haja na umuhimu wa kuwajengea uwezo Wazanzibari katika kuzifahamu vyema huduma za mafao ya fidia kazini ili kuweza kutoa haki kwa mfanyakazi ama wategemezi wao pindi mfanyakazi atakapopata ajali akiwa kazini.
Katika kikao hicho Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar ameshuhudia utiaji wa saini kati ya WCF na ZSSF ya makubaliano ya kufanya kazi kwa ushirikiano jambo ambalo litaleta tija na mafanikio makubwa kwa wafanya kazi wa pande zote mbili za jamuhuri ya muungano wa Tanzania
DKT SAMIA:TUNAFANYA UCHAGUZI KWA FEDHA ZETU WENYEWE
24-10-2025
MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MANYARA
24-10-2025
π¨ππππ£πππππ πͺπ πππ§. π¦ππ ππ π¨π ππππ§π ππ ππ‘π ππͺπ πͺππ£ππ‘πππ‘π, πͺππππ¨ππππ πππ
πππ©πππͺ ππ πͺπͺ πΏπ π©. πππππ§π€ ππ¬ππ₯π€π ππ πππ€π£ππ€π―π π¬π πΎππΌπΏπππΌ π£π πΌπΎπ
24-10-2025
πππ§. π¦ππ ππ ππ§π¨π π‘πππ‘π π¬π ππ₯πππ π¬π ππππ’π π
24-10-2025
KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. ASHA-ROSE MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR
24-10-2025
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025-2030
24-10-2025
WASIRA:CCM HATUKATI MGOMBEA ILA TUNATEUA WACHACHE KATI YA WENGI
24-10-2025
WANACHAMA 280 WA CHADEMA WATIMKIA CCM
24-10-2025
BALOZI NCHIMBI: MAONI YOYOTE KUHUSU AMANI YA TANZANIA HAYATAPUUZWA
24-10-2025
π¦ππ₯πππππ π¬π π₯πππ¦ πππ§. π¦ππ ππ ππ ππͺπππ ππππ π π¬π π πππ‘πππππ’ ππππ π¦ππππ π¨ - ππ£π. ππ π’π¦ π ππππππ
24-10-2025
MAKALLA: BARABARA YA MPWAPWA NJIAPANDA KONGWA KUJENGWA LAMI
24-10-2025
BALOZI NCHIMBI AWASILI ARUSHA
24-10-2025
TAARIFA KWA UMMA
24-10-2025
UCHAGUZI MKUU SIO AJALI-WASIRA
24-10-2025
πͺπππ¨π ππ π π¦ππππππ¨π π©ππ’π‘ππ’ππ ππππππππ ππͺππ‘π¬π ππ¨π₯π ππ π ππ’π‘π - (π ππ) πππ©π¨
24-10-2025
MONGELLA AONGOZA MAZISHI YA KADA WA CCM JIJINI MWANZA
24-10-2025
ASIYETII SHERIA, KATIBA NA KUWA TAYARI KUUA KWA MASLAHI BINAFSI HUO NI UGAIDI’
24-10-2025
πππ π¬ππ¦ππ¦ππ§πππ πͺπππ’π πππ ππ¨πππππππͺπ ππͺπ ππ¨πππ‘πππ§ππ π¨πͺπππ’, π¨πππππ‘ππ’ π‘π π¨πππππππ¨, π¬ππππ ππ π πππ¨π‘ππ - πππ. πππ©π¨
24-10-2025
KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA
24-10-2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji na uchakataji pamba cha MOLI Oil Mills Co. Ltd kilichopo Bariadi Mkoani Simiyu tarehe 16 Juni, 2025.
24-10-2025